< תְהִלִּים 145 >
תְּהִלָּ֗ה לְדָ֫וִ֥ד אֲרֹומִמְךָ֣ אֱלֹוהַ֣י הַמֶּ֑לֶךְ וַאֲבָרֲכָ֥ה שִׁ֝מְךָ֗ לְעֹולָ֥ם וָעֶֽד׃ | 1 |
Wimbo wa Sifa. Wa Daudi. Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, nitalisifu jina lako milele na milele.
בְּכָל־יֹ֥ום אֲבָרֲכֶ֑ךָּ וַאֲהַלְלָ֥ה שִׁ֝מְךָ֗ לְעֹולָ֥ם וָעֶֽד׃ | 2 |
Kila siku nitakusifu na kulitukuza jina lako milele na milele.
גָּ֘דֹ֤ול יְהוָ֣ה וּמְהֻלָּ֣ל מְאֹ֑ד וְ֝לִגְדֻלָּתֹ֗ו אֵ֣ין חֵֽקֶר׃ | 3 |
Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, ukuu wake haupimiki.
דֹּ֣ור לְ֭דֹור יְשַׁבַּ֣ח מַעֲשֶׂ֑יךָ וּגְב֖וּרֹתֶ֣יךָ יַגִּֽידוּ׃ | 4 |
Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, watasimulia matendo yako makuu.
הֲ֭דַר כְּבֹ֣וד הֹודֶ֑ךָ וְדִבְרֵ֖י נִפְלְאֹותֶ֣יךָ אָשִֽׂיחָה׃ | 5 |
Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.
וֶעֱז֣וּז נֹורְאֹתֶ֣יךָ יֹאמֵ֑רוּ וּגְדוּלֹּתֶיךָ (וּגְדוּלָּתְךָ֥) אֲסַפְּרֶֽנָּה׃ | 6 |
Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, nami nitatangaza matendo yako makuu.
זֵ֣כֶר רַב־טוּבְךָ֣ יַבִּ֑יעוּ וְצִדְקָתְךָ֥ יְרַנֵּֽנוּ׃ | 7 |
Wataadhimisha wema wako mwingi, na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.
חַנּ֣וּן וְרַח֣וּם יְהוָ֑ה אֶ֥רֶךְ אַ֝פַּ֗יִם וּגְדָל־חָֽסֶד׃ | 8 |
Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.
טֹוב־יְהוָ֥ה לַכֹּ֑ל וְ֝רַחֲמָ֗יו עַל־כָּל־מַעֲשָֽׂיו׃ | 9 |
Bwana ni mwema kwa wote, ana huruma kwa vyote alivyovifanya.
יֹוד֣וּךָ יְ֭הוָה כָּל־מַעֲשֶׂ֑יךָ וַ֝חֲסִידֶ֗יךָ יְבָרֲכֽוּכָה׃ | 10 |
Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, watakatifu wako watakutukuza.
כְּבֹ֣וד מַלְכוּתְךָ֣ יֹאמֵ֑רוּ וּגְבוּרָתְךָ֥ יְדַבֵּֽרוּ׃ | 11 |
Watasimulia utukufu wa ufalme wako na kusema juu ya ukuu wako,
לְהֹודִ֤יעַ ׀ לִבְנֵ֣י הָ֭אָדָם גְּבוּרֹתָ֑יו וּ֝כְבֹ֗וד הֲדַ֣ר מַלְכוּתֹֽו׃ | 12 |
ili watu wote wajue matendo yako makuu na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
מַֽלְכוּתְךָ֗ מַלְכ֥וּת כָּל־עֹֽלָמִ֑ים וּ֝מֶֽמְשֶׁלְתְּךָ֗ בְּכָל־דֹּ֥ור וָדֹֽור׃ | 13 |
Ufalme wako ni ufalme wa milele, mamlaka yako hudumu vizazi vyote. Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
סֹומֵ֣ךְ יְ֭הוָה לְכָל־הַנֹּפְלִ֑ים וְ֝זֹוקֵ֗ף לְכָל־הַכְּפוּפִֽים׃ | 14 |
Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.
עֵֽינֵי־כֹ֭ל אֵלֶ֣יךָ יְשַׂבֵּ֑רוּ וְאַתָּ֤ה נֹֽותֵן־לָהֶ֖ם אֶת־אָכְלָ֣ם בְּעִתֹּֽו׃ | 15 |
Macho yao wote yanakutazama wewe, nawe huwapa chakula chao wakati wake.
פֹּותֵ֥חַ אֶת־יָדֶ֑ךָ וּמַשְׂבִּ֖יעַ לְכָל־חַ֣י רָצֹֽון׃ | 16 |
Waufumbua mkono wako, watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.
צַדִּ֣יק יְ֭הוָה בְּכָל־דְּרָכָ֑יו וְ֝חָסִ֗יד בְּכָל־מַעֲשָֽׂיו׃ | 17 |
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
קָרֹ֣וב יְ֭הוָה לְכָל־קֹרְאָ֑יו לְכֹ֤ל אֲשֶׁ֖ר יִקְרָאֻ֣הוּ בֶאֱמֶֽת׃ | 18 |
Bwana yu karibu na wote wamwitao, karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.
רְצֹון־יְרֵאָ֥יו יַעֲשֶׂ֑ה וְֽאֶת־שַׁוְעָתָ֥ם יִ֝שְׁמַ֗ע וְיֹושִׁיעֵֽם׃ | 19 |
Huwatimizia wamchao matakwa yao, husikia kilio chao na kuwaokoa.
שֹׁומֵ֣ר יְ֭הוָה אֶת־כָּל־אֹהֲבָ֑יו וְאֵ֖ת כָּל־הָרְשָׁעִ֣ים יַשְׁמִֽיד׃ | 20 |
Bwana huwalinda wote wampendao, bali waovu wote atawaangamiza.
תְּהִלַּ֥ת יְהוָ֗ה יְֽדַבֶּ֫ר־פִּ֥י וִיבָרֵ֣ךְ כָּל־בָּ֭שָׂר שֵׁ֥ם קָדְשֹׁ֗ו לְעֹולָ֥ם וָעֶֽד׃ | 21 |
Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana. Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu milele na milele.