< תהילים 96 >

שירו ליהוה שיר חדש שירו ליהוה כל-הארץ 1
Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
שירו ליהוה ברכו שמו בשרו מיום-ליום ישועתו 2
Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
ספרו בגוים כבודו בכל-העמים נפלאותיו 3
Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
כי גדול יהוה ומהלל מאד נורא הוא על-כל-אלהים 4
Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
כי כל-אלהי העמים אלילים ויהוה שמים עשה 5
Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
הוד-והדר לפניו עז ותפארת במקדשו 6
Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
הבו ליהוה משפחות עמים הבו ליהוה כבוד ועז 7
Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
הבו ליהוה כבוד שמו שאו-מנחה ובאו לחצרותיו 8
Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
השתחוו ליהוה בהדרת-קדש חילו מפניו כל-הארץ 9
Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
אמרו בגוים יהוה מלך-- אף-תכון תבל בל-תמוט ידין עמים במישרים 10
Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
ישמחו השמים ותגל הארץ ירעם הים ומלאו 11
Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
יעלז שדי וכל-אשר-בו אז ירננו כל-עצי-יער 12
Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
לפני יהוה כי בא-- כי בא לשפט הארץ ישפט-תבל בצדק ועמים באמונתו 13
mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.

< תהילים 96 >