< תהילים 76 >

למנצח בנגינת מזמור לאסף שיר ב נודע ביהודה אלהים בישראל גדול שמו 1
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
ויהי בשלם סוכו ומעונתו בציון 2
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
שמה שבר רשפי-קשת מגן וחרב ומלחמה סלה 3
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
נאור אתה אדיר-- מהררי-טרף 4
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
אשתוללו אבירי לב-- נמו שנתם ולא-מצאו כל-אנשי-חיל ידיהם 5
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
מגערתך אלהי יעקב נרדם ורכב וסוס 6
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
אתה נורא אתה--ומי-יעמד לפניך מאז אפך 7
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
משמים השמעת דין ארץ יראה ושקטה 8
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
בקום-למשפט אלהים-- להושיע כל-ענוי-ארץ סלה 9
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
כי-חמת אדם תודך שארית חמת תחגר 10
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
נדרו ושלמו ליהוה אלהיכם כל-סביביו--יבילו שי למורא 11
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
יבצר רוח נגידים נורא למלכי-ארץ 12
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.

< תהילים 76 >