< תהילים 73 >

מזמור לאסף אך טוב לישראל אלהים-- לברי לבב 1
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
ואני--כמעט נטוי (נטיו) רגלי כאין שפכה (שפכו) אשרי 2
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
כי-קנאתי בהוללים שלום רשעים אראה 3
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
כי אין חרצבות למותם ובריא אולם 4
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
בעמל אנוש אינמו ועם-אדם לא ינגעו 5
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
לכן ענקתמו גאוה יעטף-שית חמס למו 6
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
יצא מחלב עינמו עברו משכיות לבב 7
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
ימיקו וידברו ברע עשק ממרום ידברו 8
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
שתו בשמים פיהם ולשונם תהלך בארץ 9
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
לכן ישיב (ישוב) עמו הלם ומי מלא ימצו למו 10
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
ואמרו איכה ידע-אל ויש דעה בעליון 11
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
הנה-אלה רשעים ושלוי עולם השגו-חיל 12
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
אך-ריק זכיתי לבבי וארחץ בנקיון כפי 13
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
ואהי נגוע כל-היום ותוכחתי לבקרים 14
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
אם-אמרתי אספרה כמו הנה דור בניך בגדתי 15
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
ואחשבה לדעת זאת עמל היא (הוא) בעיני 16
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
עד-אבוא אל-מקדשי-אל אבינה לאחריתם 17
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
אך בחלקות תשית למו הפלתם למשואות 18
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
איך היו לשמה כרגע ספו תמו מן-בלהות 19
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
כחלום מהקיץ-- אדני בעיר צלמם תבזה 20
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
כי יתחמץ לבבי וכליותי אשתונן 21
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
ואני-בער ולא אדע בהמות הייתי עמך 22
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
ואני תמיד עמך אחזת ביד-ימיני 23
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
בעצתך תנחני ואחר כבוד תקחני 24
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
מי-לי בשמים ועמך לא-חפצתי בארץ 25
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
כלה שארי ולבבי צור-לבבי וחלקי--אלהים לעולם 26
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
כי-הנה רחקיך יאבדו הצמתה כל-זונה ממך 27
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
ואני קרבת אלהים-- לי-טוב שתי באדני יהוה מחסי לספר כל-מלאכותיך 28
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< תהילים 73 >