< תהילים 73 >
מזמור לאסף אך טוב לישראל אלהים-- לברי לבב | 1 |
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
ואני--כמעט נטוי (נטיו) רגלי כאין שפכה (שפכו) אשרי | 2 |
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
כי-קנאתי בהוללים שלום רשעים אראה | 3 |
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
כי אין חרצבות למותם ובריא אולם | 4 |
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
בעמל אנוש אינמו ועם-אדם לא ינגעו | 5 |
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
לכן ענקתמו גאוה יעטף-שית חמס למו | 6 |
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
יצא מחלב עינמו עברו משכיות לבב | 7 |
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
ימיקו וידברו ברע עשק ממרום ידברו | 8 |
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
שתו בשמים פיהם ולשונם תהלך בארץ | 9 |
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
לכן ישיב (ישוב) עמו הלם ומי מלא ימצו למו | 10 |
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
ואמרו איכה ידע-אל ויש דעה בעליון | 11 |
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
הנה-אלה רשעים ושלוי עולם השגו-חיל | 12 |
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
אך-ריק זכיתי לבבי וארחץ בנקיון כפי | 13 |
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
ואהי נגוע כל-היום ותוכחתי לבקרים | 14 |
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
אם-אמרתי אספרה כמו הנה דור בניך בגדתי | 15 |
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
ואחשבה לדעת זאת עמל היא (הוא) בעיני | 16 |
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
עד-אבוא אל-מקדשי-אל אבינה לאחריתם | 17 |
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
אך בחלקות תשית למו הפלתם למשואות | 18 |
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
איך היו לשמה כרגע ספו תמו מן-בלהות | 19 |
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
כחלום מהקיץ-- אדני בעיר צלמם תבזה | 20 |
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
כי יתחמץ לבבי וכליותי אשתונן | 21 |
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
ואני-בער ולא אדע בהמות הייתי עמך | 22 |
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
ואני תמיד עמך אחזת ביד-ימיני | 23 |
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
בעצתך תנחני ואחר כבוד תקחני | 24 |
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
מי-לי בשמים ועמך לא-חפצתי בארץ | 25 |
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
כלה שארי ולבבי צור-לבבי וחלקי--אלהים לעולם | 26 |
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
כי-הנה רחקיך יאבדו הצמתה כל-זונה ממך | 27 |
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
ואני קרבת אלהים-- לי-טוב שתי באדני יהוה מחסי לספר כל-מלאכותיך | 28 |
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.