< תהילים 71 >

בך-יהוה חסיתי אל-אבושה לעולם 1
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
בצדקתך תצילני ותפלטני הטה-אלי אזנך והושיעני 2
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
היה לי לצור מעון לבוא-- תמיד צוית להושיעני כי-סלעי ומצודתי אתה 3
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
אלהי--פלטני מיד רשע מכף מעול וחומץ 4
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
כי-אתה תקותי אדני יהוה מבטחי מנעורי 5
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
עליך נסמכתי מבטן--ממעי אמי אתה גוזי בך תהלתי תמיד 6
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
כמופת הייתי לרבים ואתה מחסי-עז 7
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
ימלא פי תהלתך כל-היום תפארתך 8
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
אל-תשליכני לעת זקנה ככלות כחי אל-תעזבני 9
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
כי-אמרו אויבי לי ושמרי נפשי נועצו יחדו 10
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
לאמר אלהים עזבו רדפו ותפשוהו כי-אין מציל 11
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
אלהים אל-תרחק ממני אלהי לעזרתי חישה (חושה) 12
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
יבשו יכלו שטני נפשי יעטו חרפה וכלמה--מבקשי רעתי 13
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
ואני תמיד איחל והוספתי על-כל-תהלתך 14
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
פי יספר צדקתך--כל-היום תשועתך כי לא ידעתי ספרות 15
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
אבוא--בגברות אדני יהוה אזכיר צדקתך לבדך 16
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
אלהים למדתני מנעורי ועד-הנה אגיד נפלאותיך 17
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
וגם עד-זקנה ושיבה-- אלהים אל-תעזבני עד-אגיד זרועך לדור לכל-יבוא גבורתך 18
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
וצדקתך אלהים עד-מרום אשר-עשית גדלות אלהים מי כמוך 19
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
אשר הראיתנו (הראיתני) צרות רבות-- ורעות תשוב תחינו (תחיני) ומתהמות הארץ תשוב תעלני 20
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
תרב גדלתי ותסב תנחמני 21
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
גם-אני אודך בכלי-נבל-- אמתך אלהי אזמרה לך בכנור-- קדוש ישראל 22
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
תרננה שפתי כי אזמרה-לך ונפשי אשר פדית 23
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
גם-לשוני-- כל-היום תהגה צדקתך כי-בשו כי-חפרו מבקשי רעתי 24
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< תהילים 71 >