< תהילים 69 >
למנצח על-שושנים לדוד ב הושיעני אלהים-- כי באו מים עד-נפש | 1 |
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
טבעתי ביון מצולה-- ואין מעמד באתי במעמקי-מים ושבלת שטפתני | 2 |
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
יגעתי בקראי נחר גרוני כלו עיני--מיחל לאלהי | 3 |
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
רבו משערות ראשי-- שנאי חנם עצמו מצמיתי איבי שקר-- אשר לא-גזלתי אז אשיב | 4 |
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
אלהים--אתה ידעת לאולתי ואשמותי ממך לא-נכחדו | 5 |
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
אל-יבשו בי קויך-- אדני יהוה צבאות אל-יכלמו בי מבקשיך-- אלהי ישראל | 6 |
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
כי-עליך נשאתי חרפה כסתה כלמה פני | 7 |
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
מוזר הייתי לאחי ונכרי לבני אמי | 8 |
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
כי-קנאת ביתך אכלתני וחרפות חורפיך נפלו עלי | 9 |
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
ואבכה בצום נפשי ותהי לחרפות לי | 10 |
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
ואתנה לבושי שק ואהי להם למשל | 11 |
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
ישיחו בי ישבי שער ונגינות שותי שכר | 12 |
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
ואני תפלתי-לך יהוה עת רצון-- אלהים ברב-חסדך ענני באמת ישעך | 13 |
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
הצילני מטיט ואל-אטבעה אנצלה משנאי וממעמקי מים | 14 |
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
אל-תשטפני שבלת מים-- ואל-תבלעני מצולה ואל-תאטר-עלי באר פיה | 15 |
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
ענני יהוה כי-טוב חסדך כרב רחמיך פנה אלי | 16 |
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
ואל-תסתר פניך מעבדך כי-צר-לי מהר ענני | 17 |
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
קרבה אל-נפשי גאלה למען איבי פדני | 18 |
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
אתה ידעת--חרפתי ובשתי וכלמתי נגדך כל-צוררי | 19 |
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
חרפה שברה לבי-- ואנושה ואקוה לנוד ואין ולמנחמים ולא מצאתי | 20 |
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
ויתנו בברותי ראש ולצמאי ישקוני חמץ | 21 |
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
יהי-שלחנם לפניהם לפח ולשלומים למוקש | 22 |
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
תחשכנה עיניהם מראות ומתניהם תמיד המעד | 23 |
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
שפך-עליהם זעמך וחרון אפך ישיגם | 24 |
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
תהי-טירתם נשמה באהליהם אל-יהי ישב | 25 |
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
כי-אתה אשר-הכית רדפו ואל-מכאוב חלליך יספרו | 26 |
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
תנה-עון על-עונם ואל-יבאו בצדקתך | 27 |
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
ימחו מספר חיים ועם צדיקים אל-יכתבו | 28 |
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
ואני עני וכואב ישועתך אלהים תשגבני | 29 |
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
אהללה שם-אלהים בשיר ואגדלנו בתודה | 30 |
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
ותיטב ליהוה משור פר מקרן מפריס | 31 |
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
ראו ענוים ישמחו דרשי אלהים ויחי לבבכם | 32 |
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
כי-שמע אל-אביונים יהוה ואת-אסיריו לא בזה | 33 |
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
יהללוהו שמים וארץ ימים וכל-רמש בם | 34 |
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
כי אלהים יושיע ציון ויבנה ערי יהודה וישבו שם וירשוה | 35 |
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
וזרע עבדיו ינחלוה ואהבי שמו ישכנו-בה | 36 |
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.