< תהילים 33 >

רננו צדיקים ביהוה לישרים נאוה תהלה 1
Furahini katika Yahwe, ninyi wenye haki; kusifu kwa wenye haki kwa faa sana.
הודו ליהוה בכנור בנבל עשור זמרו-לו 2
Mshukuruni Bwana kwa kinubi; mwimbieni sifa kwa kinubi chenye nyuzi kumi.
שירו-לו שיר חדש היטיבו נגן בתרועה 3
Mwimbieni yeye wimbo mpaya; pigeni kwa ustadi na muimbe kwa furaha.
כי-ישר דבר-יהוה וכל-מעשהו באמונה 4
Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
אהב צדקה ומשפט חסד יהוה מלאה הארץ 5
Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
בדבר יהוה שמים נעשו וברוח פיו כל-צבאם 6
Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
כנס כנד מי הים נתן באוצרות תהומות 7
Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
ייראו מיהוה כל-הארץ ממנו יגורו כל-ישבי תבל 8
Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
כי הוא אמר ויהי הוא-צוה ויעמד 9
Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.
יהוה הפיר עצת-גוים הניא מחשבות עמים 10
Yahwe huvunja muungano wa mataifa; naye huishinda mipango ya wanadamu.
עצת יהוה לעולם תעמד מחשבות לבו לדר ודר 11
Mipango ya Yahwe husimama milele, mipango ya moyo wake ni kwa ajili ya vizazi vyote.
אשרי הגוי אשר-יהוה אלהיו העם בחר לנחלה לו 12
Limebarikiwa taifa ambalo Mungu wao ni Yahwe, watu ambao yeye amewachagua kama warithi wake.
משמים הביט יהוה ראה את-כל-בני האדם 13
Yahwe anatazama kutoka mbinguni; yeye huona watu wote.
ממכון-שבתו השגיח-- אל כל-ישבי הארץ 14
Kutokea mahali ambapo yeye anaishi, huwatazama wote waishio juu ya nchi.
היצר יחד לבם המבין אל-כל-מעשיהם 15
Yeye anaye iumba mioyo yao na kuyaona matendo yao yote.
אין-המלך נושע ברב-חיל גבור לא-ינצל ברב-כח 16
Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa; shujaa haokolewi na nguvu zake nyingi.
שקר הסוס לתשועה וברב חילו לא ימלט 17
Farasi sio salama kwa ajili ya ushindi; ijapokuwa nguvu zake ni nyingi, hawezi kuokoa.
הנה עין יהוה אל-יראיו למיחלים לחסדו 18
Tazama, macho ya Yahwe yako kwa wale wanao mhofu yeye, wale wanao litumainia agano lake takatifu
להציל ממות נפשם ולחיותם ברעב 19
kuwaokoa maisha yao na mauti na kuwaweka hai wakati wa jaa.
נפשנו חכתה ליהוה עזרנו ומגננו הוא 20
Sisi tunamngoja Yahwe, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
כי-בו ישמח לבנו כי בשם קדשו בטחנו 21
Mioyo yetu hufurahia ndani yake, kwa kuwa tunaamini katika jina lake takatifu.
יהי-חסדך יהוה עלינו כאשר יחלנו לך 22
Yahwe, agano lako takatifu, liwe pamoja nasi tuwekapo tumaini letu katika wewe.

< תהילים 33 >