< תהילים 31 >

למנצח מזמור לדוד ב בך-יהוה חסיתי אל-אבושה לעולם בצדקתך פלטני 1
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
הטה אלי אזנך-- מהרה הצילני היה לי לצור-מעוז--לבית מצודות להושיעני 2
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
כי-סלעי ומצודתי אתה ולמען שמך תנחני ותנהלני 3
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
תוציאני--מרשת זו טמנו לי כי-אתה מעוזי 4
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
בידך אפקיד רוחי פדית אותי יהוה--אל אמת 5
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
שנאתי השמרים הבלי-שוא ואני אל-יהוה בטחתי 6
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
אגילה ואשמחה בחסדך אשר ראית את-עניי ידעת בצרות נפשי 7
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
ולא הסגרתני ביד-אויב העמדת במרחב רגלי 8
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
חנני יהוה כי צר-לי עששה בכעס עיני נפשי ובטני 9
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
כי כלו ביגון חיי-- ושנותי באנחה כשל בעוני כחי ועצמי עששו 10
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
מכל-צררי הייתי חרפה ולשכני מאד-- ופחד למידעי ראי בחוץ-- נדדו ממני 11
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
נשכחתי כמת מלב הייתי ככלי אבד 12
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
כי שמעתי דבת רבים-- מגור מסביב בהוסדם יחד עלי לקחת נפשי זממו 13
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
ואני עליך בטחתי יהוה אמרתי אלהי אתה 14
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
בידך עתתי הצילני מיד-אויבי ומרדפי 15
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
האירה פניך על-עבדך הושיעני בחסדך 16
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
יהוה--אל-אבושה כי קראתיך יבשו רשעים ידמו לשאול (Sheol h7585) 17
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
תאלמנה שפתי-שקר הדברות על-צדיק עתק--בגאוה ובוז 18
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
מה רב-טובך אשר-צפנת ליראיך פעלת לחסים בך נגד בני אדם 19
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
תסתירם בסתר פניך-- מרכסי-איש תצפנם בסכה מריב לשנות 20
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
ברוך יהוה כי הפליא חסדו לי בעיר מצור 21
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
ואני אמרתי בחפזי-- נגרזתי מנגד עיניך אכן--שמעת קול תחנוני בשועי אליך 22
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
אהבו את-יהוה כל-חסידיו אמונים נצר יהוה ומשלם על-יתר עשה גאוה 23
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
חזקו ויאמץ לבבכם-- כל-המיחלים ליהוה 24
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< תהילים 31 >