< תהילים 148 >

הללו-יה הללו את-יהוה מן-השמים הללוהו במרומים 1
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
הללוהו כל-מלאכיו הללוהו כל-צבאו 2
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
הללוהו שמש וירח הללוהו כל-כוכבי אור 3
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
הללוהו שמי השמים והמים אשר מעל השמים 4
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
יהללו את-שם יהוה כי הוא צוה ונבראו 5
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
ויעמידם לעד לעולם חק-נתן ולא יעבור 6
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
הללו את-יהוה מן-הארץ-- תנינים וכל-תהמות 7
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
אש וברד שלג וקיטור רוח סערה עשה דברו 8
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
ההרים וכל-גבעות עץ פרי וכל-ארזים 9
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
החיה וכל-בהמה רמש וצפור כנף 10
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
מלכי-ארץ וכל-לאמים שרים וכל-שפטי ארץ 11
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
בחורים וגם-בתולות זקנים עם-נערים 12
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
יהללו את-שם יהוה-- כי-נשגב שמו לבדו הודו על-ארץ ושמים 13
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
וירם קרן לעמו תהלה לכל-חסידיו-- לבני ישראל עם קרבו הללו-יה 14
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< תהילים 148 >