< תהילים 141 >

מזמור לדוד יהוה קראתיך חושה לי האזינה קולי בקראי-לך 1
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
תכון תפלתי קטרת לפניך משאת כפי מנחת-ערב 2
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
שיתה יהוה שמרה לפי נצרה על-דל שפתי 3
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
אל-תט-לבי לדבר רע להתעולל עללות ברשע-- את-אישים פעלי-און ובל-אלחם במנעמיהם 4
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
יהלמני צדיק חסד ויוכיחני-- שמן ראש אל-יני ראשי כי-עוד ותפלתי ברעותיהם 5
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
נשמטו בידי-סלע שפטיהם ושמעו אמרי כי נעמו 6
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
כמו פלח ובקע בארץ-- נפזרו עצמינו לפי שאול (Sheol h7585) 7
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
כי אליך יהוה אדני עיני בכה חסיתי אל-תער נפשי 8
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
שמרני--מידי פח יקשו לי ומקשות פעלי און 9
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
יפלו במכמריו רשעים יחד אנכי עד-אעבור 10
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.

< תהילים 141 >