< תהילים 137 >

על נהרות בבל--שם ישבנו גם-בכינו בזכרנו את-ציון 1
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
על-ערבים בתוכה-- תלינו כנרותינו 2
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
כי שם שאלונו שובינו דברי-שיר-- ותוללינו שמחה שירו לנו משיר ציון 3
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
איך--נשיר את-שיר-יהוה על אדמת נכר 4
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
אם-אשכחך ירושלם-- תשכח ימיני 5
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
תדבק-לשוני לחכי-- אם-לא אזכרכי אם-לא אעלה את-ירושלם-- על ראש שמחתי 6
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
זכר יהוה לבני אדום-- את יום ירושלם האמרים ערו ערו-- עד היסוד בה 7
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
בת-בבל השדודה אשרי שישלם-לך-- את-גמולך שגמלת לנו 8
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
אשרי שיאחז ונפץ את-עלליך-- אל-הסלע 9
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.

< תהילים 137 >