< תהילים 115 >

לא לנו יהוה לא-לנו כי-לשמך תן כבוד--על-חסדך על-אמתך 1
Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi, bali utukufu ni kwa jina lako, kwa sababu ya upendo na uaminifu wako.
למה יאמרו הגוים איה-נא אלהיהם 2
Kwa nini mataifa waseme, “Yuko wapi Mungu wao?”
ואלהינו בשמים-- כל אשר-חפץ עשה 3
Mungu wetu yuko mbinguni, naye hufanya lolote limpendezalo.
עצביהם כסף וזהב מעשה ידי אדם 4
Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
פה-להם ולא ידברו עינים להם ולא יראו 5
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
אזנים להם ולא ישמעו אף להם ולא יריחון 6
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, zina pua, lakini haziwezi kunusa;
ידיהם ולא ימישון--רגליהם ולא יהלכו לא-יהגו בגרונם 7
zina mikono, lakini haziwezi kupapasa, zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala koo zao haziwezi kutoa sauti.
כמוהם יהיו עשיהם-- כל אשר-בטח בהם 8
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
ישראל בטח ביהוה עזרם ומגנם הוא 9
Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
בית אהרן בטחו ביהוה עזרם ומגנם הוא 10
Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
יראי יהוה בטחו ביהוה עזרם ומגנם הוא 11
Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana, yeye ni msaada na ngao yao.
יהוה זכרנו יברך יברך את-בית ישראל יברך את-בית אהרן 12
Bwana anatukumbuka na atatubariki: ataibariki nyumba ya Israeli, ataibariki nyumba ya Aroni,
יברך יראי יהוה-- הקטנים עם-הגדלים 13
atawabariki wale wanaomcha Bwana, wadogo kwa wakubwa.
יסף יהוה עליכם עליכם ועל בניכם 14
Bwana na awawezeshe kuongezeka, ninyi na watoto wenu.
ברוכים אתם ליהוה-- עשה שמים וארץ 15
Mbarikiwe na Bwana Muumba wa mbingu na dunia.
השמים שמים ליהוה והארץ נתן לבני-אדם 16
Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana, lakini dunia amempa mwanadamu.
לא המתים יהללו-יה ולא כל-ירדי דומה 17
Sio wafu wanaomsifu Bwana, wale washukao mahali pa kimya,
ואנחנו נברך יה-- מעתה ועד-עולם הללו-יה 18
bali ni sisi tunaomtukuza Bwana, sasa na hata milele. Msifuni Bwana.

< תהילים 115 >