< תהילים 109 >

למנצח לדוד מזמור אלהי תהלתי אל-תחרש 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
כי פי רשע ופי-מרמה--עלי פתחו דברו אתי לשון שקר 2
kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
ודברי שנאה סבבוני וילחמוני חנם 3
Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
תחת-אהבתי ישטנוני ואני תפלה 4
Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
וישימו עלי רעה תחת טובה ושנאה תחת אהבתי 5
Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
הפקד עליו רשע ושטן יעמד על-ימינו 6
Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
בהשפטו יצא רשע ותפלתו תהיה לחטאה 7
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
יהיו-ימיו מעטים פקדתו יקח אחר 8
Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
יהיו-בניו יתומים ואשתו אלמנה 9
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
ונוע ינועו בניו ושאלו ודרשו מחרבותיהם 10
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
ינקש נושה לכל-אשר-לו ויבזו זרים יגיעו 11
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
אל-יהי-לו משך חסד ואל-יהי חונן ליתומיו 12
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
יהי-אחריתו להכרית בדור אחר ימח שמם 13
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
יזכר עון אבתיו--אל-יהוה וחטאת אמו אל-תמח 14
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
יהיו נגד-יהוה תמיד ויכרת מארץ זכרם 15
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
יען-- אשר לא זכר עשות חסד וירדף איש-עני ואביון--ונכאה לבב למותת 16
Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
ויאהב קללה ותבואהו ולא-חפץ בברכה ותרחק ממנו 17
Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
וילבש קללה כמדו ותבא כמים בקרבו וכשמן בעצמותיו 18
Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
תהי-לו כבגד יעטה ולמזח תמיד יחגרה 19
Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
זאת פעלת שטני מאת יהוה והדברים רע על-נפשי 20
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
ואתה יהוה אדני-- עשה-אתי למען שמך כי-טוב חסדך הצילני 21
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
כי-עני ואביון אנכי ולבי חלל בקרבי 22
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
כצל-כנטותו נהלכתי ננערתי כארבה 23
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
ברכי כשלו מצום ובשרי כחש משמן 24
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
ואני הייתי חרפה להם יראוני יניעון ראשם 25
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
עזרני יהוה אלהי הושיעני כחסדך 26
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
וידעו כי-ידך זאת אתה יהוה עשיתה 27
Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
יקללו-המה ואתה תברך קמו ויבשו--ועבדך ישמח 28
Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
ילבשו שוטני כלמה ויעטו כמעיל בשתם 29
Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
אודה יהוה מאד בפי ובתוך רבים אהללנו 30
Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
כי-יעמד לימין אביון-- להושיע משפטי נפשו 31
Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

< תהילים 109 >