< מִשְׁלֵי 5 >

בני לחכמתי הקשיבה לתבונתי הט-אזנך 1
Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu, sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,
לשמר מזמות ודעת שפתיך ינצרו 2
ili uweze kutunza busara na midomo yako ihifadhi maarifa.
כי נפת תטפנה שפתי זרה וחלק משמן חכה 3
Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
ואחריתה מרה כלענה חדה כחרב פיות 4
lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.
רגליה ירדות מות שאול צעדיה יתמכו (Sheol h7585) 5
Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini. (Sheol h7585)
ארח חיים פן-תפלס נעו מעגלתיה לא תדע 6
Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
ועתה בנים שמעו-לי ואל-תסורו מאמרי-פי 7
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.
הרחק מעליה דרכך ואל-תקרב אל-פתח ביתה 8
Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
פן-תתן לאחרים הודך ושנתיך לאכזרי 9
usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,
פן-ישבעו זרים כחך ועצביך בבית נכרי 10
wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.
ונהמת באחריתך בכלות בשרך ושארך 11
Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
ואמרת--איך שנאתי מוסר ותוכחת נאץ לבי 12
Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!
ולא-שמעתי בקול מורי ולמלמדי לא-הטיתי אזני 13
Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.
כמעט הייתי בכל-רע-- בתוך קהל ועדה 14
Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa katikati ya kusanyiko lote.”
שתה-מים מבורך ונזלים מתוך בארך 15
Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.
יפוצו מעינתיך חוצה ברחבות פלגי-מים 16
Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?
יהיו-לך לבדך ואין לזרים אתך 17
Na viwe vyako mwenyewe, kamwe visishirikishwe wageni.
יהי-מקורך ברוך ושמח מאשת נעורך 18
Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
אילת אהבים ויעלת-חן דדיה ירוך בכל-עת באהבתה תשגה תמיד 19
Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.
ולמה תשגה בני בזרה ותחבק חק נכריה 20
Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?
כי נכח עיני יהוה--דרכי-איש וכל-מעגלתיו מפלס 21
Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.
עוונתיו--ילכדנו את-הרשע ובחבלי חטאתו יתמך 22
Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.
הוא--ימות באין מוסר וברב אולתו ישגה 23
Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.

< מִשְׁלֵי 5 >