< מִשְׁלֵי 25 >

גם-אלה משלי שלמה-- אשר העתיקו אנשי חזקיה מלך-יהודה 1
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
כבד אלהים הסתר דבר וכבד מלכים חקר דבר 2
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
שמים לרום וארץ לעמק ולב מלכים אין חקר 3
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
הגו סיגים מכסף ויצא לצרף כלי 4
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
הגו רשע לפני-מלך ויכון בצדק כסאו 5
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
אל-תתהדר לפני-מלך ובמקום גדלים אל-תעמד 6
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
כי טוב אמר-לך עלה-הנה מהשפילך לפני נדיב--אשר ראו עיניך 7
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
אל-תצא לרב מהר פן מה-תעשה באחריתה--בהכלים אתך רעך 8
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
ריבך ריב את-רעך וסוד אחר אל-תגל 9
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
פן-יחסדך שמע ודבתך לא תשוב 10
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
תפוחי זהב במשכיות כסף-- דבר דבר על-אפניו 11
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
נזם זהב וחלי-כתם-- מוכיח חכם על-אזן שמעת 12
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
כצנת שלג ביום קציר--ציר נאמן לשלחיו ונפש אדניו ישיב 13
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
נשיאים ורוח וגשם אין-- איש מתהלל במתת-שקר 14
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
בארך אפים יפתה קצין ולשון רכה תשבר-גרם 15
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
דבש מצאת אכל דיך פן-תשבענו והקאתו 16
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
הקר רגלך מבית רעך פן-ישבעך ושנאך 17
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
מפיץ וחרב וחץ שנון-- איש ענה ברעהו עד שקר 18
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
שן רעה ורגל מועדת-- מבטח בוגד ביום צרה 19
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
מעדה-בגד ביום קרה--חמץ על-נתר ושר בשרים על לב-רע 20
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
אם-רעב שנאך האכלהו לחם ואם-צמא השקהו מים 21
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
כי גחלים--אתה חתה על-ראשו ויהוה ישלם-לך 22
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
רוח צפון תחולל גשם ופנים נזעמים לשון סתר 23
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
טוב שבת על-פנת-גג-- מאשת מדונים (מדינים) ובית חבר 24
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
מים קרים על-נפש עיפה ושמועה טובה מארץ מרחק 25
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
מעין נרפש ומקור משחת-- צדיק מט לפני-רשע 26
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
אכל דבש הרבות לא-טוב וחקר כבדם כבוד 27
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
עיר פרוצה אין חומה-- איש אשר אין מעצר לרוחו 28
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< מִשְׁלֵי 25 >