< איכה 3 >
אני הגבר ראה עני בשבט עברתו | 1 |
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
אותי נהג וילך חשך ולא אור | 2 |
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
אך בי ישב יהפך ידו כל היום | 3 |
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
בלה בשרי ועורי שבר עצמותי | 4 |
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
במחשכים הושיבני כמתי עולם | 6 |
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
גדר בעדי ולא אצא הכביד נחשתי | 7 |
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
גם כי אזעק ואשוע שתם תפלתי | 8 |
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
גדר דרכי בגזית נתיבתי עוה | 9 |
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
דב ארב הוא לי אריה (ארי) במסתרים | 10 |
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
דרכי סורר ויפשחני שמני שמם | 11 |
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
דרך קשתו ויציבני כמטרא לחץ | 12 |
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
הייתי שחק לכל עמי נגינתם כל היום | 14 |
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
השביעני במרורים הרוני לענה | 15 |
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
ויגרס בחצץ שני הכפישני באפר | 16 |
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
ותזנח משלום נפשי נשיתי טובה | 17 |
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
ואמר אבד נצחי ותוחלתי מיהוה | 18 |
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
זכר עניי ומרודי לענה וראש | 19 |
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
זכור תזכור ותשיח (ותשוח) עלי נפשי | 20 |
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
זאת אשיב אל לבי על כן אוחיל | 21 |
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
חסדי יהוה כי לא תמנו כי לא כלו רחמיו | 22 |
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
חדשים לבקרים רבה אמונתך | 23 |
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
חלקי יהוה אמרה נפשי על כן אוחיל לו | 24 |
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
טוב יהוה לקוו לנפש תדרשנו | 25 |
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
טוב ויחיל ודומם לתשועת יהוה | 26 |
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
טוב לגבר כי ישא על בנעוריו | 27 |
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
ישב בדד וידם כי נטל עליו | 28 |
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
יתן בעפר פיהו אולי יש תקוה | 29 |
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
יתן למכהו לחי ישבע בחרפה | 30 |
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
כי אם הוגה ורחם כרב חסדיו | 32 |
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
כי לא ענה מלבו ויגה בני איש | 33 |
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
לדכא תחת רגליו כל אסירי ארץ | 34 |
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
להטות משפט גבר נגד פני עליון | 35 |
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
לעות אדם בריבו אדני לא ראה | 36 |
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
מי זה אמר ותהי אדני לא צוה | 37 |
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
מפי עליון לא תצא הרעות והטוב | 38 |
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
מה יתאונן אדם חי גבר על חטאו | 39 |
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
נחפשה דרכינו ונחקרה ונשובה עד יהוה | 40 |
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
נשא לבבנו אל כפים אל אל בשמים | 41 |
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
נחנו פשענו ומרינו אתה לא סלחת | 42 |
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
סכותה באף ותרדפנו הרגת לא חמלת | 43 |
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
סכותה בענן לך מעבור תפלה | 44 |
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
סחי ומאוס תשימנו בקרב העמים | 45 |
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
פצו עלינו פיהם כל איבינו | 46 |
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
פחד ופחת היה לנו השאת והשבר | 47 |
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
פלגי מים תרד עיני על שבר בת עמי | 48 |
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
עיני נגרה ולא תדמה מאין הפגות | 49 |
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
עד ישקיף וירא יהוה משמים | 50 |
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
עיני עוללה לנפשי מכל בנות עירי | 51 |
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
צוד צדוני כצפור איבי חנם | 52 |
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
צמתו בבור חיי וידו אבן בי | 53 |
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
צפו מים על ראשי אמרתי נגזרתי | 54 |
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
קראתי שמך יהוה מבור תחתיות | 55 |
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
קולי שמעת אל תעלם אזנך לרוחתי לשועתי | 56 |
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
קרבת ביום אקראך אמרת אל תירא | 57 |
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
רבת אדני ריבי נפשי גאלת חיי | 58 |
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
ראיתה יהוה עותתי שפטה משפטי | 59 |
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
ראיתה כל נקמתם--כל מחשבתם לי | 60 |
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
שמעת חרפתם יהוה כל מחשבתם עלי | 61 |
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
שפתי קמי והגיונם עלי כל היום | 62 |
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
שבתם וקימתם הביטה אני מנגינתם | 63 |
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
תשיב להם גמול יהוה כמעשה ידיהם | 64 |
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
תתן להם מגנת לב תאלתך להם | 65 |
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
תרדף באף ותשמידם מתחת שמי יהוה | 66 |
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.