< איכה 3 >

אני הגבר ראה עני בשבט עברתו 1
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
אותי נהג וילך חשך ולא אור 2
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
אך בי ישב יהפך ידו כל היום 3
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
בלה בשרי ועורי שבר עצמותי 4
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
בנה עלי ויקף ראש ותלאה 5
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
במחשכים הושיבני כמתי עולם 6
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
גדר בעדי ולא אצא הכביד נחשתי 7
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
גם כי אזעק ואשוע שתם תפלתי 8
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
גדר דרכי בגזית נתיבתי עוה 9
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
דב ארב הוא לי אריה (ארי) במסתרים 10
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
דרכי סורר ויפשחני שמני שמם 11
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
דרך קשתו ויציבני כמטרא לחץ 12
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
הביא בכליתי בני אשפתו 13
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
הייתי שחק לכל עמי נגינתם כל היום 14
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
השביעני במרורים הרוני לענה 15
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
ויגרס בחצץ שני הכפישני באפר 16
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
ותזנח משלום נפשי נשיתי טובה 17
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
ואמר אבד נצחי ותוחלתי מיהוה 18
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
זכר עניי ומרודי לענה וראש 19
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
זכור תזכור ותשיח (ותשוח) עלי נפשי 20
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
זאת אשיב אל לבי על כן אוחיל 21
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
חסדי יהוה כי לא תמנו כי לא כלו רחמיו 22
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
חדשים לבקרים רבה אמונתך 23
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
חלקי יהוה אמרה נפשי על כן אוחיל לו 24
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
טוב יהוה לקוו לנפש תדרשנו 25
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
טוב ויחיל ודומם לתשועת יהוה 26
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
טוב לגבר כי ישא על בנעוריו 27
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
ישב בדד וידם כי נטל עליו 28
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
יתן בעפר פיהו אולי יש תקוה 29
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
יתן למכהו לחי ישבע בחרפה 30
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
כי לא יזנח לעולם אדני 31
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
כי אם הוגה ורחם כרב חסדיו 32
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
כי לא ענה מלבו ויגה בני איש 33
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
לדכא תחת רגליו כל אסירי ארץ 34
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
להטות משפט גבר נגד פני עליון 35
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
לעות אדם בריבו אדני לא ראה 36
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
מי זה אמר ותהי אדני לא צוה 37
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
מפי עליון לא תצא הרעות והטוב 38
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
מה יתאונן אדם חי גבר על חטאו 39
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
נחפשה דרכינו ונחקרה ונשובה עד יהוה 40
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
נשא לבבנו אל כפים אל אל בשמים 41
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
נחנו פשענו ומרינו אתה לא סלחת 42
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
סכותה באף ותרדפנו הרגת לא חמלת 43
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
סכותה בענן לך מעבור תפלה 44
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
סחי ומאוס תשימנו בקרב העמים 45
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
פצו עלינו פיהם כל איבינו 46
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
פחד ופחת היה לנו השאת והשבר 47
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
פלגי מים תרד עיני על שבר בת עמי 48
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
עיני נגרה ולא תדמה מאין הפגות 49
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
עד ישקיף וירא יהוה משמים 50
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
עיני עוללה לנפשי מכל בנות עירי 51
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
צוד צדוני כצפור איבי חנם 52
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
צמתו בבור חיי וידו אבן בי 53
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
צפו מים על ראשי אמרתי נגזרתי 54
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
קראתי שמך יהוה מבור תחתיות 55
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
קולי שמעת אל תעלם אזנך לרוחתי לשועתי 56
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
קרבת ביום אקראך אמרת אל תירא 57
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
רבת אדני ריבי נפשי גאלת חיי 58
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
ראיתה יהוה עותתי שפטה משפטי 59
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
ראיתה כל נקמתם--כל מחשבתם לי 60
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
שמעת חרפתם יהוה כל מחשבתם עלי 61
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
שפתי קמי והגיונם עלי כל היום 62
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
שבתם וקימתם הביטה אני מנגינתם 63
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
תשיב להם גמול יהוה כמעשה ידיהם 64
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
תתן להם מגנת לב תאלתך להם 65
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
תרדף באף ותשמידם מתחת שמי יהוה 66
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.

< איכה 3 >