< איוב 33 >

ואולם--שמע-נא איוב מלי וכל-דברי האזינה 1
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
הנה-נא פתחתי פי דברה לשוני בחכי 2
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
ישר-לבי אמרי ודעת שפתי ברור מללו 3
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
רוח-אל עשתני ונשמת שדי תחיני 4
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
אם-תוכל השיבני ערכה לפני התיצבה 5
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
הן-אני כפיך לאל מחמר קרצתי גם-אני 6
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
הנה אמתי לא תבעתך ואכפי עליך לא-יכבד 7
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
אך אמרת באזני וקול מלין אשמע 8
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
זך אני בלי-פשע חף אנכי ולא עון לי 9
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
הן תנואות עלי ימצא יחשבני לאויב לו 10
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
ישם בסד רגלי ישמר כל-ארחתי 11
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
הן-זאת לא-צדקת אענך כי-ירבה אלוה מאנוש 12
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
מדוע אליו ריבות כי כל-דבריו לא יענה 13
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
כי-באחת ידבר-אל ובשתים לא ישורנה 14
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
בחלום חזיון לילה--בנפל תרדמה על-אנשים בתנומות עלי משכב 15
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
אז יגלה אזן אנשים ובמסרם יחתם 16
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
להסיר אדם מעשה וגוה מגבר יכסה 17
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
יחשך נפשו מני-שחת וחיתו מעבר בשלח 18
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
והוכח במכאוב על-משכבו וריב (ורוב) עצמיו אתן 19
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
וזהמתו חיתו לחם ונפשו מאכל תאוה 20
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
יכל בשרו מראי ושפי (ושפו) עצמתיו לא ראו 21
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
ותקרב לשחת נפשו וחיתו לממתים 22
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
אם-יש עליו מלאך--מליץ אחד מני-אלף להגיד לאדם ישרו 23
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
ויחננו--ויאמר פדעהו מרדת שחת מצאתי כפר 24
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
רטפש בשרו מנער ישוב לימי עלומיו 25
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
יעתר אל-אלוה וירצהו וירא פניו בתרועה וישב לאנוש צדקתו 26
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
ישר על-אנשים ויאמר חטאתי וישר העויתי ולא-שוה לי 27
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
פדה נפשי (נפשו) מעבר בשחת וחיתי (וחיתו) באור תראה 28
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
הן-כל-אלה יפעל-אל-- פעמים שלוש עם-גבר 29
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
להשיב נפשו מני-שחת-- לאור באור החיים 30
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
הקשב איוב שמע-לי החרש ואנכי אדבר 31
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
אם-יש-מלין השיבני דבר כי-חפצתי צדקך 32
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
אם-אין אתה שמע-לי החרש ואאלפך חכמה 33
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< איוב 33 >