< איוב 30 >

ועתה שחקו עלי-- צעירים ממני לימים אשר-מאסתי אבותם-- לשית עם-כלבי צאני 1
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
גם-כח ידיהם למה לי עלימו אבד כלח 2
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
בחסר ובכפן גלמוד הערקים ציה--אמש שואה ומשאה 3
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
הקטפים מלוח עלי-שיח ושרש רתמים לחמם 4
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
מן-גו יגרשו יריעו עלימו כגנב 5
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
בערוץ נחלים לשכן חרי עפר וכפים 6
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
בין-שיחים ינהקו תחת חרול יספחו 7
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
בני-נבל גם-בני בלי-שם-- נכאו מן-הארץ 8
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
ועתה נגינתם הייתי ואהי להם למלה 9
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
תעבוני רחקו מני ומפני לא-חשכו רק 10
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
כי-יתרו (יתרי) פתח ויענני ורסן מפני שלחו 11
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
על-ימין פרחח יקומו רגלי שלחו ויסלו עלי ארחות אידם 12
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
נתסו נתיבתי להותי יעילו לא עזר למו 13
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
כפרץ רחב יאתיו תחת שאה התגלגלו 14
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
ההפך עלי בלהות תרדף כרוח נדבתי וכעב עברה ישעתי 15
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
ועתה--עלי תשתפך נפשי יאחזוני ימי-עני 16
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
לילה--עצמי נקר מעלי וערקי לא ישכבון 17
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
ברב-כח יתחפש לבושי כפי כתנתי יאזרני 18
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
הרני לחמר ואתמשל כעפר ואפר 19
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
אשוע אליך ולא תענני עמדתי ותתבנן בי 20
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
תהפך לאכזר לי בעצם ידך תשטמני 21
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
תשאני אל-רוח תרכיבני ותמגגני תשוה (תשיה) 22
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
כי-ידעתי מות תשיבני ובית מועד לכל-חי 23
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
אך לא-בעי ישלח-יד אם-בפידו להן שוע 24
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
אם-לא בכיתי לקשה-יום עגמה נפשי לאביון 25
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
כי טוב קויתי ויבא רע ואיחלה לאור ויבא אפל 26
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
מעי רתחו ולא-דמו קדמני ימי-עני 27
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
קדר הלכתי בלא חמה קמתי בקהל אשוע 28
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
אח הייתי לתנים ורע לבנות יענה 29
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
עורי שחר מעלי ועצמי-חרה מני-חרב 30
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
ויהי לאבל כנרי ועגבי לקול בכים 31
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< איוב 30 >