< איוב 17 >

רוחי חבלה ימי נזעכו קברים לי 1
Moyo wangu umevunjika, siku zangu zimefupishwa, kaburi linaningojea.
אם-לא התלים עמדי ובהמרותם תלן עיני 2
Hakika wenye mizaha wamenizunguka; macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.
שימה-נא ערבני עמך מי הוא לידי יתקע 3
“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai. Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?
כי-לבם צפנת משכל על-כן לא תרמם 4
Umezifunga akili zao zisipate ufahamu, kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.
לחלק יגיד רעים ועיני בניו תכלנה 5
Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
והציגני למשל עמים ותפת לפנים אהיה 6
“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu, mtu ambaye watu humtemea mate usoni.
ותכה מכעש עיני ויצרי כצל כלם 7
Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi; umbile langu lote ni kama kivuli.
ישמו ישרים על-זאת ונקי על-חנף יתערר 8
Watu wanyofu wanatishwa na hili; watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.
ויאחז צדיק דרכו וטהר-ידים יסיף אמץ 9
Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao, nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.
ואולם--כלם תשבו ובאו נא ולא-אמצא בכם חכם 10
“Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena! Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.
ימי עברו זמתי נתקו-- מורשי לבבי 11
Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika, vivyo hivyo shauku za moyo wangu.
לילה ליום ישימו אור קרוב מפני-חשך 12
Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana, kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’
אם-אקוה שאול ביתי בחשך רפדתי יצועי (Sheol h7585) 13
Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, kama nikikitandika kitanda changu gizani, (Sheol h7585)
לשחת קראתי אבי אתה אמי ואחתי לרמה 14
kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’ na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’
ואיה אפו תקותי ותקותי מי ישורנה 15
liko wapi basi tarajio langu? Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?
בדי שאל תרדנה אם-יחד על-עפר נחת (Sheol h7585) 16
Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? Je, tutashuka pamoja mavumbini?” (Sheol h7585)

< איוב 17 >