< איוב 17 >
רוחי חבלה ימי נזעכו קברים לי | 1 |
Moyo wangu umevunjika, siku zangu zimefupishwa, kaburi linaningojea.
אם-לא התלים עמדי ובהמרותם תלן עיני | 2 |
Hakika wenye mizaha wamenizunguka; macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.
שימה-נא ערבני עמך מי הוא לידי יתקע | 3 |
“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai. Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?
כי-לבם צפנת משכל על-כן לא תרמם | 4 |
Umezifunga akili zao zisipate ufahamu, kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.
לחלק יגיד רעים ועיני בניו תכלנה | 5 |
Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
והציגני למשל עמים ותפת לפנים אהיה | 6 |
“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu, mtu ambaye watu humtemea mate usoni.
ותכה מכעש עיני ויצרי כצל כלם | 7 |
Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi; umbile langu lote ni kama kivuli.
ישמו ישרים על-זאת ונקי על-חנף יתערר | 8 |
Watu wanyofu wanatishwa na hili; watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.
ויאחז צדיק דרכו וטהר-ידים יסיף אמץ | 9 |
Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao, nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.
ואולם--כלם תשבו ובאו נא ולא-אמצא בכם חכם | 10 |
“Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena! Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.
ימי עברו זמתי נתקו-- מורשי לבבי | 11 |
Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika, vivyo hivyo shauku za moyo wangu.
לילה ליום ישימו אור קרוב מפני-חשך | 12 |
Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana, kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’
אם-אקוה שאול ביתי בחשך רפדתי יצועי (Sheol ) | 13 |
Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, kama nikikitandika kitanda changu gizani, (Sheol )
לשחת קראתי אבי אתה אמי ואחתי לרמה | 14 |
kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’ na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’
ואיה אפו תקותי ותקותי מי ישורנה | 15 |
liko wapi basi tarajio langu? Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?
בדי שאל תרדנה אם-יחד על-עפר נחת (Sheol ) | 16 |
Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? Je, tutashuka pamoja mavumbini?” (Sheol )