< איוב 15 >

ויען אליפז התימני ויאמר 1
Kisha Elifazi Mtemani akajibu:
החכם יענה דעת-רוח וימלא קדים בטנו 2
“Je, mtu mwenye hekima hujibu kwa mawazo matupu, au kujaza tumbo lake kwa upepo wenye joto wa mashariki?
הוכח בדבר לא-יסכון ומלים לא-יועיל בם 3
Je, aweza kubishana juu ya maneno yasiyofaa, kwa hotuba zisizo na maana?
אף-אתה תפר יראה ותגרע שיחה לפני-אל 4
Lakini unadhoofisha hata uchaji wa Mungu na kuzuia ibada mbele za Mungu.
כי יאלף עונך פיך ותבחר לשון ערומים 5
Dhambi yako inasukuma kinywa chako, nawe umechagua ulimi wa hila.
ירשיעך פיך ולא-אני ושפתיך יענו-בך 6
Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si changu; midomo yako mwenyewe inashuhudia dhidi yako.
הראישון אדם תולד ולפני גבעות חוללת 7
“Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa? Ulizaliwa kabla ya vilima?
הבסוד אלוה תשמע ותגרע אליך חכמה 8
Je, wewe husikiliza mashauri ya siri ya Mungu? Je, wewe unaizuia hekima iwe yako mwenyewe?
מה-ידעת ולא נדע תבין ולא-עמנו הוא 9
Wewe unajua kitu gani tusichokijua sisi? Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
גם-שב גם-ישיש בנו-- כביר מאביך ימים 10
Wale wenye mvi na wazee wako upande wetu, watu ambao ni wazee hata kuliko baba yako.
המעט ממך תנחומות אל ודבר לאט עמך 11
Je, faraja za Mungu hazikutoshi, au maneno yaliyosemwa kwako kwa upole si kitu?
מה-יקחך לבך ומה-ירזמון עיניך 12
Kwa nini moyo wako unakudanganya, na kwa nini macho yako yanangʼaa,
כי-תשיב אל-אל רוחך והצאת מפיך מלין 13
ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu, na kumwaga maneno kama hayo kutoka kinywani mwako?
מה-אנוש כי-יזכה וכי-יצדק ילוד אשה 14
“Mwanadamu ni kitu gani, hata aweze kuwa safi, au yeye aliyezaliwa na mwanamke, hata aweze kuwa mwadilifu?
הן בקדשו לא יאמין ושמים לא-זכו בעיניו 15
Kama Mungu hawaamini watakatifu wake, kama hata mbingu zenyewe si safi machoni pake,
אף כי-נתעב ונאלח איש-שתה כמים עולה 16
sembuse mwanadamu ambaye ni mwovu na mpotovu, ambaye hunywa uovu kama anywavyo maji!
אחוך שמע-לי וזה-חזיתי ואספרה 17
“Nisikilize mimi nami nitakueleza, acha nikuambie yale niliyoyaona,
אשר-חכמים יגידו ולא כחדו מאבותם 18
ambayo watu wenye hekima wameyanena, bila kuficha lolote walilopokea toka kwa baba zao
להם לבדם נתנה הארץ ולא-עבר זר בתוכם 19
(wakati ambao wao peke yao ndio walipewa nchi, hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao):
כל-ימי רשע הוא מתחולל ומספר שנים נצפנו לעריץ 20
Mtu mwovu siku zake zote hupata mateso, miaka yote aliwekewa mkorofi.
קול-פחדים באזניו בשלום שודד יבואנו 21
Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake; katika kufanikiwa kwake, wanyangʼanyi humshambulia.
לא-יאמין שוב מני-חשך וצפו (וצפוי) הוא אלי-חרב 22
Hukata tamaa kuokoka gizani; amewekwa kwa ajili ya upanga.
נדד הוא ללחם איה ידע כי-נכון בידו יום-חשך 23
Hutangatanga, akitafuta chakula; anajua kwamba siku ya giza iko karibu.
יבעתהו צר ומצוקה תתקפהו כמלך עתיד לכידור 24
Taabu na maumivu makuu vinamtia hofu; humshinda kama mfalme aliye tayari kwa vita,
כי-נטה אל-אל ידו ואל-שדי יתגבר 25
kwa sababu amemkunjia Mungu ngumi yake na kujigamba dhidi ya Mwenyezi,
ירוץ אליו בצואר בעבי גבי מגניו 26
kwa kiburi akishambulia dhidi ya Mungu akiwa na ngao nene, iliyo imara.
כי-כסה פניו בחלבו ויעש פימה עלי-כסל 27
“Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene na kiuno chake kimevimba kwa kunenepa,
וישכון ערים נכחדות--בתים לא-ישבו למו אשר התעתדו לגלים 28
ataishi katika miji ya magofu, na katika nyumba ambazo haziishi mwanadamu yeyote, nyumba zinazokuwa vifusi.
לא-יעשר ולא-יקום חילו ולא-יטה לארץ מנלם 29
Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu, wala mali zake hazitakuwa nyingi juu ya nchi.
לא-יסור מני-חשך--ינקתו תיבש שלהבת ויסור ברוח פיו 30
Hatatoka gizani; mwali wa moto utanyausha machipukizi yake, nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.
אל-יאמן בשו נתעה כי-שוא תהיה תמורתו 31
Asijidanganye mwenyewe kutumainia ubatili, kwa kuwa hatapata malipo yoyote.
בלא-יומו תמלא וכפתו לא רעננה 32
Atakuwa amelipwa kikamilifu kabla ya wakati wake, nayo matawi yake hayatastawi.
יחמס כגפן בסרו וישלך כזית נצתו 33
Atafanana na mzabibu uliopukutishwa matunda yake kabla hayajaiva, kama mzeituni unaodondosha maua yake.
כי-עדת חנף גלמוד ואש אכלה אהלי-שחד 34
Kwa kuwa jamii ya wasiomcha Mungu watakuwa tasa, nao moto utateketeza hema za wale wanaopenda rushwa.
הרה עמל וילד און ובטנם תכין מרמה 35
Hutunga mimba ya madhara na kuzaa uovu; matumbo yao huumba udanganyifu.”

< איוב 15 >