< בראשית 40 >

ויהי אחר הדברים האלה חטאו משקה מלך מצרים והאפה--לאדניהם למלך מצרים 1
Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
ויקצף פרעה על שני סריסיו--על שר המשקים ועל שר האופים 2
Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
ויתן אתם במשמר בית שר הטבחים--אל בית הסהר מקום אשר יוסף אסור שם 3
akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
ויפקד שר הטבחים את יוסף אתם--וישרת אתם ויהיו ימים במשמר 4
Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
ויחלמו חלום שניהם איש חלמו בלילה אחד--איש כפתרון חלמו המשקה והאפה אשר למלך מצרים אשר אסורים בבית הסהר 5
kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
ויבא אליהם יוסף בבקר וירא אתם והנם זעפים 6
Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
וישאל את סריסי פרעה אשר אתו במשמר בית אדניו--לאמר מדוע פניכם רעים היום 7
Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
ויאמרו אליו--חלום חלמנו ופתר אין אתו ויאמר אלהם יוסף הלוא לאלהים פתרנים--ספרו נא לי 8
Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
ויספר שר המשקים את חלמו ליוסף ויאמר לו--בחלומי והנה גפן לפני 9
Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
ובגפן שלשה שריגם והוא כפרחת עלתה נצה הבשילו אשכלתיה ענבים 10
nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
וכוס פרעה בידי ואקח את הענבים ואשחט אתם אל כוס פרעה ואתן את הכוס על כף פרעה 11
Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
ויאמר לו יוסף זה פתרנו שלשת השרגים--שלשת ימים הם 12
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
בעוד שלשת ימים ישא פרעה את ראשך והשיבך על כנך ונתת כוס פרעה בידו כמשפט הראשון אשר היית משקהו 13
Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
כי אם זכרתני אתך כאשר ייטב לך ועשית נא עמדי חסד והזכרתני אל פרעה והוצאתני מן הבית הזה 14
Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
כי גנב גנבתי מארץ העברים וגם פה לא עשיתי מאומה כי שמו אתי בבור 15
Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
וירא שר האפים כי טוב פתר ויאמר אל יוסף אף אני בחלומי והנה שלשה סלי חרי על ראשי 16
Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
ובסל העליון מכל מאכל פרעה--מעשה אפה והעוף אכל אתם מן הסל--מעל ראשי 17
Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
ויען יוסף ויאמר זה פתרנו שלשת הסלים--שלשת ימים הם 18
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
בעוד שלשת ימים ישא פרעה את ראשך מעליך ותלה אותך על עץ ואכל העוף את בשרך מעליך 19
Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
ויהי ביום השלישי יום הלדת את פרעה ויעש משתה לכל עבדיו וישא את ראש שר המשקים ואת ראש שר האפים--בתוך עבדיו 20
Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
וישב את שר המשקים על משקהו ויתן הכוס על כף פרעה 21
Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
ואת שר האפים תלה כאשר פתר להם יוסף 22
lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
ולא זכר שר המשקים את יוסף וישכחהו 23
Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.

< בראשית 40 >