< דברי הימים א 23 >

ודויד זקן ושבע ימים וימלך את שלמה בנו על ישראל 1
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
ויאסף את כל שרי ישראל והכהנים והלוים 2
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
ויספרו הלוים מבן שלשים שנה ומעלה ויהי מספרם לגלגלתם לגברים שלשים ושמונה אלף 3
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
מאלה לנצח על מלאכת בית יהוה עשרים וארבעה אלף ושטרים ושפטים ששת אלפים 4
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
וארבעת אלפים שערים וארבעת אלפים מהללים ליהוה בכלים אשר עשיתי להלל 5
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
ויחלקם דויד מחלקות לבני לוי לגרשון קהת ומררי 6
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
לגרשני לעדן ושמעי 7
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
בני לעדן הראש יחיאל וזתם ויואל--שלשה 8
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
בני שמעי שלמות (שלמית) וחזיאל והרן--שלשה אלה ראשי האבות ללעדן 9
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
ובני שמעי--יחת זינא ויעוש ובריעה אלה בני שמעי ארבעה 10
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
ויהי יחת הראש וזיזה השני ויעוש ובריעה לא הרבו בנים ויהיו לבית אב לפקדה אחת 11
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
בני קהת עמרם יצהר חברון ועזיאל--ארבעה 12
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
בני עמרם אהרן ומשה ויבדל אהרן להקדישו קדש קדשים הוא ובניו עד עולם--להקטיר לפני יהוה לשרתו ולברך בשמו עד עולם 13
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
ומשה איש האלהים--בניו יקראו על שבט הלוי 14
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
בני משה גרשום ואליעזר 15
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
בני גרשום שבואל הראש 16
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
ויהיו בני אליעזר רחביה הראש ולא היה לאליעזר בנים אחרים ובני רחביה רבו למעלה 17
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
בני יצהר שלמית הראש 18
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
בני חברון--יריהו הראש אמריה השני יחזיאל השלישי ויקמעם הרביעי 19
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
בני עזיאל--מיכה הראש וישיה השני 20
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
בני מררי מחלי ומושי בני מחלי אלעזר וקיש 21
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
וימת אלעזר ולא היו לו בנים כי אם בנות וישאום בני קיש אחיהם 22
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
בני מושי מחלי ועדר וירמות--שלושה 23
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
אלה בני לוי לבית אבותיהם ראשי האבות לפקודיהם במספר שמות לגלגלתם עשה המלאכה לעבדת בית יהוה--מבן עשרים שנה ומעלה 24
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
כי אמר דויד הניח יהוה אלהי ישראל לעמו וישכן בירושלם עד לעולם 25
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
וגם ללוים--אין לשאת את המשכן ואת כל כליו לעבדתו 26
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
כי בדברי דויד האחרונים המה מספר בני לוי מבן עשרים שנה ולמעלה 27
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
כי מעמדם ליד בני אהרן לעבדת בית יהוה על החצרות ועל הלשכות ועל טהרת לכל קדש--ומעשה עבדת בית האלהים 28
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
וללחם המערכת ולסלת למנחה ולרקיקי המצות ולמחבת ולמרבכת ולכל משורה ומדה 29
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
ולעמד בבקר בבקר להדות ולהלל ליהוה וכן לערב 30
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
ולכל העלות עלות ליהוה לשבתות לחדשים ולמעדים--במספר כמשפט עליהם תמיד לפני יהוה 31
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
ושמרו את משמרת אהל מועד ואת משמרת הקדש ומשמרת בני אהרן אחיהם--לעבדת בית יהוה 32
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< דברי הימים א 23 >