< Hesekiel 38 >

1 Und es geschah Jehovahs Wort zu mir, sprechend:
Neno la Yahwe likanijia, likisema,
2 Menschensohn, richte dein Angesicht gegen Gog, das Land Magog, den Fürsten, das Haupt von Meschech und Thubal, und weissage wider ihn,
“Mwanadamu, weka uso wako kumwelekea Gogu, nchi ya Magogu, kiongozi mkuu wa Mesheki na Tubali; na kutabiri dhidi yake.
3 Und sprich: So spricht der Herr Jehovah: Siehe, Ich bin wider dich, Gog, du Fürst, Haupt von Meschech und Thubal,
Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Ni juu yako, Gogu, kiongozi mkuu wa Mesheki na Tubali.
4 Und Ich wende dich zurück und tue Haken in deine Kinnbacken und bringe heraus dich und all deine Streitmacht, Rosse und Reiter, alle vollkommen gekleidet, eine große Versammlung mit Schild und Tartsche, allesamt fassend die Schwerter.
Hivyo nitakugeuza na kuweka kulabu kwenye taya yako; nitakupeleka nje pamoja na jeshi lako lote, farasi, na waendesha farasi, wote wakiwa wamevaa silaha, kusanyiko kubwa pamoja na ngao ndogo na ngao kubwa, wote wakishikilia panga!
5 Perser, Kusch und Pud mit ihnen, sie alle mit Tartsche und Helm.
Persia, Kushi, Uajemi wapo pamoja nao, wote pamoja na ngao na chapeo!
6 Gomer und alle seine Scharen, Beth Thogarmah, an den Seiten der Mitternacht, und alle seine Scharen, viele Völker mit dir.
Gomeri na jeshi lake lote, na Beth-Togarma, kutoka sehemu za mbali ya kaskazini, na jeshi lake lote! Watu wengi wako pamoja nawe!
7 Sei bereit und bereite dich, du und alle deine Versammlung, die sich um dich angesammelt, und sei ihnen zur Hut.
Kuwa tayari! Ndio, jiandae na jeshi lako waliokusanyika pamoja na wewe, na amiri wao mkuu.
8 Nach vielen Tagen wirst du heimgesucht werden, in der Zukunft Jahren wirst du kommen in ein Land, das vom Schwert zurückgebracht aus vielen Völkern zusammengebracht worden, auf die Berge Israels, die beständig eine Öde gewesen, das aus den Völkern herausgebracht worden ist, und wohnen allesamt sicher.
Utaitwa baada ya siku nyingi, na baada ya miaka michache utaenda kwenye nchi iliyofunikwa kutoka upanga na ambayo iliyokusanywa kutoka watu wengi, iliyowkusanya kuwarudisha milima ya Israeli ambayo imeendelea kuangamizwa. Lakini watu wa nchi watatolewa na kabila za watu, na wataishi salama, wote!
9 Und wie ein Unwetter ziehst du herauf, du kommst, wie eine Wolke, das Land zu bedecken wirst du sein, du und all deine Scharen, und viele Völker mit dir.
Hivyo utapanda juu kama tufani iendavyo; utakuwa kama wingu lililofunika nchi, wewe na jeshi lako lote, maaskari wako wote pamoja na wewe.
10 So spricht der Herr Jehovah: Und geschehen wird an jenem Tag, daß Dinge in dein Herz aufsteigen und du böse Gedanken denkst,
Bwana Yahwe asema hivi: Itakuwa siku hiyo hayo mawazo yataingia moyoni mwako, na utatunga njama mbaya.'
11 Und sprichst: Ich will hinaufziehen in ein offenliegendes Land, will kommen zu denen, die rasten, die wohnen in Sicherheit. Sie alle wohnen ohne Mauer und Riegel, und Torflügel haben sie keine.
Kisha utasema, 'nitapanda hata nchi iliyowazi; nitaenda hata kwa watu wapole waishio salama, wote wakiishi mahali ambapo hakuna kuta wala makomeo, na mahali ambapo hakuna malango ya mji.
12 Um Beute zu erbeuten und Raub zu rauben, und deine Hand zurückzukehren wider die Öden, die bewohnt sind, und wider ein Volk, das aus den Völkerschaften ist gesammelt worden, und Viehherden und Habe sich schafft und wohnt im Nabel der Erde.
Nitanyakua mateka na kuiba mateka, ili nilete mkono wangu juu kuwaangamiza wale wakazi wapya, na juu ya watu waliokusanyika kutoka mataifa, watu wale waongezao wanyama na mali, na wale waishio katikatika ya dunia.'
13 Scheba und Dedan und die Händler von Tharschisch und alle seine jungen Löwen werden zu dir sagen: Bist du gekommen Beute zu erbeuten, um Raub zu rauben, hast deine Versammlung du angesammelt, auf daß du Silber und Gold wegtragest, Viehherde und Habe wegnehmest, um große Beute zu erbeuten?
Sheba na Denani, na wafanya biashara wa Tarshishi pamoja na mahodari wake wote watakwambia, 'Je, umekuja kuteka nyara? Je, umewakusanya majeshi yako kuchukua mateka, kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua mifugo yao na mali na kuwakokota mateka wengi sana?'
14 Darum weissage, Menschensohn, und sprich zu Gog: So spricht der Herr Jehovah: Wirst du nicht an jenem Tag es wissen, daß Mein Volk Israel wohnt in Sicherheit?
Kwa hiyo tabiri, mwanadamu, na mwambie Gogu, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku hiyo, wakati watu wangu Israeli watakapoishi salama, je, hutajifunza kuhusu wao?
15 Und du kommst von deinem Ort, von den Seiten der Mitternacht, du und viele Völker mit dir, sie alle auf Rossen reitend, eine große Versammlung und viele Streitmacht.
Utakuja kutoka mahali pangu mbali katika kaskazini pamoja na jeshi kubwa, wote wakiendesha farasi, kusanyiko kubwa, jeshi kubwa.
16 Und ziehst herauf wider Mein Volk Israel, wie eine Wolke das Land zu bedecken. In der Zukunft der Tage wird es geschehen, daß Ich dich in Mein Land hereinbringe, auf daß die Völkerschaften Mich erkennen, wie Ich Mich durch dich, o Gog, vor ihren Augen heilige.
Utawashambulia watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Katika siku za baadaye nitakuleta juu ya nchi yangu, ili mataifa wanijue nitakapojifunua mwenyewe kupitia wewe, Gogu, kuwa mtakatifu mbele ya macho yao.
17 So spricht der Herr Jehovah: Bist du es, von dem Ich in den Tagen der Vorzeit durch die Hand Meiner Knechte, der Propheten Israels, geredet habe, die in jenen Tagen jahrelang weissagten, daß Ich dich wider sie hereinbringen würde?
Bwana Yahwe asema hivi: Je, wewe siye yule ambaye niliyeongea naye katika siku za zamani kwa mkono wa watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri katika mda wao wenyewe kwa miaka niliyowaleta juu yao?
18 Und wird geschehen an selbigem Tage, am Tage, da Gog auf den Boden Israels kommt, sagt der Herr Jehovah, daß Mein Grimm aufsteigt in Meinem Zorn.
Basi itakuwa katika siku hiyo wakati Gogu atakapo ishambulia nchi ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-ghadhabu yangu itapanda katika hasira yangu.
19 Und in Meinem Eifer, im Feuer Meines Wütens, rede Ich: Fürwahr, an jenem Tage wird ein großes Erdbeben sein auf dem Boden Israels,
Katika wivu wangu katika hasira ya moto wangu, ninasema kwamba katika siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la nchi katika nchi ya Israeli.
20 Daß vor Meinem Angesicht beben die Fische des Meeres und der Himmel Gevögel und das wilde Tier des Feldes und all das Kriechtier, das auf dem Boden kriecht, und jeder Mensch auf den Angesichten des Bodens; und Berge werden umgerissen und Felsenwände fallen und zur Erde fällt jede Mauer.
Watatetemeka mbele yangu-samaki wa baharini na ndege wa angani, wanyama wa mashambani, na viumbe watambaao juu ya nchi, na kila mtu aliyeko juu ya uso wa nchi. Milima itaangushwa chini majabali yataanguka, hadi kila ukuta utaanguka kwenye nchi.
21 Und Ich rufe wider ihn auf allen Meinen Bergen das Schwert, spricht der Herr Jehovah, das Schwert des Mannes soll wider seinen Bruder sein.
Nitaita upanga dhidi yake juu ya milima yangu yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-upanga wa kila mtu utakuwa kinyume na ndugu yake.
22 Und Ich will mit ihm rechten mit Pest und mit Blut, und mit überflutendem Platzregen; und Steine des Hagels, Feuer und Schwefel, lasse Ich regnen über ihn und über seine Scharen, und über die vielen Völker, die mit ihm sind.
Kisha nitamuhukumu kwa tauni na damu; nakufurika mvua na mvua ya mawe na kuchoma asidi nitainyeshea chini juu yake na jeshi lake na mataifa mengi yaliyo pamoja naye.
23 Und Ich erweise Mich groß und heilige Mich, und tue Mich kund vor den Augen vieler Völkerschaften, auf daß sie wissen, daß Ich Jehovah bin.
Kwa kuwa nitaonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu na nitafanya kujulikana mimi mwenyewe katiaka macho ya mataifa mengi, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.”

< Hesekiel 38 >