< Hohelied 1 >

1 Das Lied der Lieder, von Salomo.
Wimbo ulio bora wa Solomoni.
2 Er küsse mich mit seines Mundes Küssen; denn lieblicher als Wein ist deine Liebe.
Unibusu kwa busu la kinywa chako, kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.
3 Lieblich duften deine Salben; wie ausgegossenes Öl ist dein Name, darum haben dich Jungfrauen lieb.
Manukato yako yananukia vizuri, jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa. Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!
4 Zieh mich dir nach; o, laß uns eilen! - mich führte der König in seine Gemächer - Wir wollen jubeln und uns deiner freuen, deine Liebe preisen mehr als den Wein; mit Recht lieben sie dich!
Nichukue twende nawe, na tufanye haraka! Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake. Marafiki Tunakushangilia na kukufurahia, tutasifu upendo wako zaidi kuliko divai. Mpendwa Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!
5 Schwarz bin ich, doch lieblich, ihr Töchter Jerusalems! wie Kedars Gezelte, wie Salomos Zeltdecken.
Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi binti za Yerusalemu, mweusi kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya hema la Solomoni.
6 Seht mich nicht an, daß ich so schwärzlich bin, daß die Sonne mich verbrannt hat. Die Söhne meiner Mutter zürnten auf mich; sie bestellten mich zur Weinbergshüterin - meinen eigenen Weinberg habe ich nicht gehütet!
Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu nimefanywa mweusi na jua. Wana wa mama yangu walinikasirikia na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu. Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.
7 Thu' mir kund, o du, den meine Seele liebt: Wo weidest du? wo lagerst du am Mittag? Denn warum soll ich wie eine Vermummte sein bei den Herden deiner Genossen?
Niambie, wewe ambaye ninakupenda, unalisha wapi kundi lako la kondoo na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela karibu na makundi ya rafiki zako?
8 Wenn du's nicht weißt, o du schönste unter den Frauen, so geh' doch hinaus den Spuren der Herde nach und weide deine Zicklein bei den Hütten der Hirten.
Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote, fuata nyayo za kondoo, na kulisha wana-mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
9 Den Stuten am Pharaowagen vergleiche ich dich, meine Freundin.
Mpenzi wangu, ninakufananisha na farasi jike aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.
10 Lieblich stehn deinen Wangen die Gehänge, deinem Halse die Schnüre.
Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli, shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.
11 Gehänge von Gold wollen wir dir machen mit silbernen Punkten.
Tutakufanyia vipuli vya dhahabu, vyenye kupambwa kwa fedha.
12 So lange der König auf seinem Ruhepolster weilte, gab meine Narde ihren Duft.
Wakati mfalme alipokuwa mezani pake, manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.
13 Mein Geliebter ist mir das Balsambündel, das an meinem Busen ruht.
Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane kati ya matiti yangu.
14 Die Cyprusdolde in Engedis Weinbergen ist mein Geliebter mir.
Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.
15 Wie schön bist du, meine Freundin; wie schön bist du! Deine Augen sind Taubenaugen.
Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Tazama jinsi ulivyo mzuri! Macho yako ni kama ya hua.
16 Wie schön bist du, mein Geliebter, ja holdselig; ja immer grün ist unser Lager.
Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, tazama jinsi unavyopendeza! Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.
17 Die Balken unseres Hauses sind Cedern, unser Getäfel Cypressen.
Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, na mapao yetu ni miberoshi.

< Hohelied 1 >