< Psalm 83 >

1 Ein Lied. Ein Psalm Asaphs. O Gott, sei nicht länger still; schweige nicht und bleibe nicht ruhig, o Gott!
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 Denn fürwahr, deine Feinde toben, und die dich hassen, erheben das Haupt.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 Wider dein Volk machen sie listigen Anschlag und beraten sich wider die von dir Geborgenen.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 Sie sprechen: “Wohlan, wir wollen sie vertilgen, daß sie kein Volk mehr seien, und des Namens Israel fortan nicht mehr gedacht werde!”
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 Denn sie haben sich einmütig beraten und schlossen einen Bund wider dich,
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 die Zelte Edoms und der Ismaeliter, Moabs und der Hagriter,
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal und Ammon und Amalek, Philistäa samt den Bewohnern von Tyrus.
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Auch Assur hat sich zu ihnen geschlagen; sie leihen den Söhnen Lots ihren Arm. (Sela)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Thue ihnen, wie Midian, wie Sisera, wie Jabin am Bache Kison.
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Sie wurden vertilgt bei Endor, wurden Dünger für das Land.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Mache sie, ihre Edlen, wie Oreb und wie Seeb und alle ihre Fürsten wie Sebah und Zalmunna.
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Sie, die da sprachen: Wir wollen für uns in Besitz nehmen die Auen Gottes!
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 Mein Gott, mache sie gleich wirbelndem Staube, gleich Stoppeln vor dem Winde.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 Wie Feuer, das den Wald entzündet, und wie eine Flamme, die Berge verbrennt,
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 so verfolge sie mit deinem Wetter und schrecke sie mit deiner Windsbraut!
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Mache ihr Angesicht voll Schmach, damit sie deinen Namen suchen, Jahwe.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Laß sie beschämt und erschreckt werden für immer; laß sie zu Schanden werden und zu Grunde gehn,
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 damit sie inne werden, daß du Jahwe heißest, du allein erhaben bist über die ganze Erde!
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalm 83 >