< Psalm 63 >

1 Ein Psalm Davids, als er in der Wüste Juda war. Gott, du bist mein Gott, dich suche ich! Es dürstet nach dir meine Seele, es schmachtet nach dir mein Leib, in dürrem, lechzendem Land ohne Wasser.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 So hab' ich dich im Heiligtume geschaut, um deine Macht und Herrlichkeit zu sehen.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Denn deine Gnade ist besser als Leben; meine Lippen sollen dich loben.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Also will ich dich preisen mein Leben lang, in deinem Namen meine Hände erheben.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Wie an Mark und Fett ersättigt sich meine Seele, und mit Jubellippen rühmt mein Mund,
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 wenn ich auf meinem Lager deiner gedenke, in den Nachtwachen über dich sinne.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Denn du warst meine Hilfe und im Schatten deiner Flügel juble ich.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Getreulich hängt dir meine Seele an; aufrecht hält mich deine Rechte.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Jene aber - zu ihrem Verderben trachten sie mir nach dem Leben; in die Tiefen der Erde werden sie hinabfahren.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Man wird ihn dem Schwerte preisgeben; der Schakale Beute werden sie.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Aber der König wird sich Gottes freuen; rühmen wird sich jeder, der bei ihm schwört, daß den Lügenrednern der Mund gestopft ward.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalm 63 >