< Psalm 52 >

1 Dem Musikmeister. Ein Maskil von David, als der Edomiter Doeg kam und Saul meldete und zu ihm sprach: David ist ins Haus Ahimelechs gekommen. Was rühmst du dich der Bosheit, du Tyrann? Die Gnade Gottes währt allezeit!
Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
2 Deine Zunge sinnt Verderben wie ein scharfes Schermesser, du Arglist Verübender!
Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
3 Du willst lieber Böses, als Gutes, redest lieber Lügen, als Wahrheit. (Sela)
Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
4 Du willst nur verderbliche Reden, nur trügerische Zunge.
Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
5 So wird dich Gott auch für immer zertrümmern, dich wegraffen und aus dem Zelte reißen und dich auswurzeln aus dem Lande der Lebendigen. (Sela)
Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
6 Die Frommen aber werden es sehen und sich fürchten und werden über ihn lachen:
Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
7 “Das ist der Mann, der Gott nicht zu seiner Schutzwehr machte, sondern sich auf seinen großen Reichtum verließ und auf seine Schätze trotzte!”
“Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
8 Ich aber bin wie ein grünender Ölbaum im Hause Gottes, verlasse mich auf Gottes Gnade immer und ewig.
Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
9 Ich will dich immerdar preisen, daß du es gethan hast, will angesichts deiner Frommen verkündigen, daß dein Name so gütig ist.
Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.

< Psalm 52 >