< Psalm 34 >

1 Von David, als er seinen Verstand vor Abimelech verstellte, und der ihn forttrieb, und er von dannen ging. Ich will Jahwe preisen alle Zeit, sein Lob soll beständig in meinem Munde sein.
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 Jahwes soll sich meine Seele rühmen; die Elenden sollen es hören und sich freuen.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 Verherrlicht Jahwe mit mir und laßt uns miteinander seinen Namen erheben!
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 So oft ich Jahwe suchte, erhörte er mich und aus allem, was ich gefürchtet, errettete er mich.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 Die auf ihn blickten, wurden leuchtenden Angesichts, und ihr Antlitz brauchte nicht zu erblassen.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 Hier ist so ein Elender, welcher rief, und Jahwe hörte und half ihm aus allen seinen Nöten.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 Der Engel Jahwes lagert sich rings um die, die ihn fürchten, und reißt sie heraus.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 Schmeckt und seht, daß Jahwe gütig ist; wohl dem Manne, der bei ihm Zuflucht sucht!
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Fürchtet Jahwe, ihr, seine Heiligen; denn die ihn fürchten, haben keinen Mangel.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 Junge Löwen darben und hungern; aber die, die Jahwe suchen, haben keinen Mangel an irgend einem Gut.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Kommt, Kinder, hört mir zu; ich will euch die Furcht Jahwes lehren!
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 Wer ist der Mann, der Leben begehrt, zahlreiche Lebenstage wünscht, um Glück zu erleben?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Wahre deine Zunge vor Bösem und deine Lippen vor trügerischer Rede!
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Halte dich fern vom Bösen und thue Gutes, suche Frieden und jage ihm nach!
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 Das Antlitz Jahwes ist wider die, die Böses thun, daß er ihr Gedächtnis von der Erde vertilge.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 Die Augen Jahwes sind auf die Frommen gerichtet, und seine Ohren auf ihr Geschrei.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 Sie schrieen und Jahwe hörte und rettete sie aus allen ihren Nöten.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 Jahwe ist denen nahe, die zerbrochenes Herzens sind, und hilft denen, die ein zerschlagenes Gemüt haben.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Zahlreich sind die Leiden des Frommen, aber Jahwe errettet ihn aus allen.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 Er behütet alle seine Gebeine, daß ihrer keines zerbrochen wird.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 Den Gottlosen wird das Unheil töten, und die den Frommen hassen, werden büßen.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 Jahwe erlöst die Seele seiner Knechte, und alle, die bei ihm Zuflucht suchen, werden nicht büßen.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Psalm 34 >