< Psalm 34 >

1 Von David, als er seinen Verstand vor Abimelech verstellte, und der ihn forttrieb, und er von dannen ging. Ich will Jahwe preisen alle Zeit, sein Lob soll beständig in meinem Munde sein.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Jahwes soll sich meine Seele rühmen; die Elenden sollen es hören und sich freuen.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Verherrlicht Jahwe mit mir und laßt uns miteinander seinen Namen erheben!
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 So oft ich Jahwe suchte, erhörte er mich und aus allem, was ich gefürchtet, errettete er mich.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Die auf ihn blickten, wurden leuchtenden Angesichts, und ihr Antlitz brauchte nicht zu erblassen.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Hier ist so ein Elender, welcher rief, und Jahwe hörte und half ihm aus allen seinen Nöten.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Der Engel Jahwes lagert sich rings um die, die ihn fürchten, und reißt sie heraus.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Schmeckt und seht, daß Jahwe gütig ist; wohl dem Manne, der bei ihm Zuflucht sucht!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Fürchtet Jahwe, ihr, seine Heiligen; denn die ihn fürchten, haben keinen Mangel.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Junge Löwen darben und hungern; aber die, die Jahwe suchen, haben keinen Mangel an irgend einem Gut.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Kommt, Kinder, hört mir zu; ich will euch die Furcht Jahwes lehren!
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Wer ist der Mann, der Leben begehrt, zahlreiche Lebenstage wünscht, um Glück zu erleben?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Wahre deine Zunge vor Bösem und deine Lippen vor trügerischer Rede!
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Halte dich fern vom Bösen und thue Gutes, suche Frieden und jage ihm nach!
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Das Antlitz Jahwes ist wider die, die Böses thun, daß er ihr Gedächtnis von der Erde vertilge.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Die Augen Jahwes sind auf die Frommen gerichtet, und seine Ohren auf ihr Geschrei.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Sie schrieen und Jahwe hörte und rettete sie aus allen ihren Nöten.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Jahwe ist denen nahe, die zerbrochenes Herzens sind, und hilft denen, die ein zerschlagenes Gemüt haben.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Zahlreich sind die Leiden des Frommen, aber Jahwe errettet ihn aus allen.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Er behütet alle seine Gebeine, daß ihrer keines zerbrochen wird.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Den Gottlosen wird das Unheil töten, und die den Frommen hassen, werden büßen.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Jahwe erlöst die Seele seiner Knechte, und alle, die bei ihm Zuflucht suchen, werden nicht büßen.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalm 34 >