< Psalm 3 >

1 Ein Psalm Davids, als er vor seinem Sohn Absalom floh. Jahwe, wie sind meiner Bedränger so viel, viele erheben sich wider mich!
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 Viele sagen von mir: Es giebt keine Hilfe für ihn bei Gott! (Sela)
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 Aber du, Jahwe, bist Schild um mich - meine Ehre und der mein Haupt erhebt!
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 Laut rief ich zu Jahwe; da erhörte er mich von seinem heiligen Berge. (Sela)
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 Ich legte mich nieder und entschlief: ich bin erwacht, denn Jahwe stützt mich.
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 Ich fürchte mich nicht vor zahllosen Scharen von Kriegsvolk, die sich ringsum wider mich gelagert haben.
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 Auf, Jahwe! Hilf mir, mein Gott! Denn du schlugst alle meine Feinde auf den Kinnbacken, zerschmettertest die Zähne der Gottlosen.
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Bei Jahwe steht die Hilfe! Über dein Volk komme dein Segen! (Sela)
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.

< Psalm 3 >