< Psalm 132 >

1 Wallfahrtslieder. Gedenke, Jahwe, David, all' seine Mühsal!
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 ihm, der Jahwe schwur, dem Starken Jakobs gelobte:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 “Ich will mein Wohngezelt nicht betreten, noch das Bett meines Lagers besteigen,
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 “will meinen Augen keinen Schlaf gönnen, meinen Wimpern keinen Schlummer,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 “bis ich für Jahwe eine Stätte gefunden, eine Wohnung für den Starken Jakobs.”
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Siehe, wir haben von ihr gehört in Ephrat, haben sie gefunden in Waldgefilden.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Laßt uns in seine Wohnung eingehen, vor dem Schemel seiner Füße niederfallen!
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Brich auf, Jahwe, nach deiner Ruhestätte, du und deine mächtige Lade!
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Deine Priester seien angethan mit rechtem Verhalten, und deine Frommen mögen jubeln!
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Um deines Knechtes Davids willen weise deinen Gesalbten nicht ab!
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Jahwe hat David einen wahrhaftigen Eid geschworen, von dem er nicht abgehen wird: “Einen, der deinem Leib entsprossen, will ich auf deinen Thron setzen!”
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Wenn deine Söhne meinen Bund beobachten und meine Zeugnisse, die ich sie lehren werde, so sollen auch ihre Söhne für immer auf deinem Throne sitzen.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Denn Jahwe hat Zion erwählt, hat es zum Wohnsitze für sich begehrt:
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 “Dies ist für immer meine Ruhestätte; hier will ich wohnen, denn nach ihr verlangte ich.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 “Ich will Zion reichlich segnen, ihre Armen mit Brot sättigen.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 “Ihre Priester will ich mit Heil bekleiden, und ihre Frommen sollen fröhlich jubeln.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 “Daselbst will ich David Macht verleihen, eine Leuchte zurichten meinem Gesalbten.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 “Seine Feinde will ich in Schande kleiden, doch auf ihm soll seine Krone glänzen!”
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalm 132 >