< Psalm 130 >

1 Wallfahrtslieder. Aus der Tiefe rufe ich dich, Jahwe,
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Herr, höre auf meine Stimme! Möchten deine Ohren aufmerksam sein auf mein lautes Flehn!
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Wenn du Verschuldungen im Gedächtnis bewahrtest, Jah, Herr, wer kann dann bestehen?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Vielmehr, bei dir steht die Vergebung, damit man dich fürchte.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 Ich harre auf Jahwe; meine Seele harrt auf sein Wort.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Innig warte ich auf den Herrn, sehnsüchtiger, als Wächter auf den Morgen, als Wächter auf den Morgen.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Harre, Israel, auf Jahwe! Denn bei Jahwe ist die Gnade und bei ihm Erlösung in Fülle,
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 und er wird Israel erlösen von allen seinen Verschuldungen.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psalm 130 >