< Psalm 129 >

1 Wallfahrtslieder. Sie haben mich viel bedrängt von meiner Jugend an - so spreche Israel! -
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
2 Sie haben mich viel bedrängt von meiner Jugend an und mich doch nicht überwältigt.
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
3 Auf meinem Rücken haben sie geackert, haben ihr Pflugland weit ausgedehnt.
Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
4 Jahwe, der gerechte, hat der Gottlosen Strang zerhauen.
Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
5 Beschämt müssen werden und zurückweichen alle, die Zion hassen.
Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
6 Sie müssen wie das Gras auf den Dächern werden, das verdorrt, bevor man es herauszieht,
Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
7 womit kein Schnitter seine Hand gefüllt, noch seinen Busen ein Garbenbinder.
ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
8 Und die des Wegs vorüberkommen, sprechen nicht: “Der Segen Jahwes sei über euch! Wir segnen euch im Namen Jahwes!”
Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”

< Psalm 129 >