< Psalm 111 >

1 Rühmet Jah! Ich will Jahwe von ganzem Herzen preisen im Kreise der Frommen und in der Gemeinde.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Groß sind die Werke Jahwes, der Erforschung wert für alle, die ihre Lust an ihnen haben.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Majestät und Hoheit ist sein Thun, und seine Gerechtigkeit besteht für immer.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 Er hat ein Gedächtnis seiner Wunder gestiftet; gnädig und barmherzig ist Jahwe.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Er hat denen, die ihn fürchten, Speise gegeben; er gedenkt auf ewig seines Bundes.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 Die Macht seines Thuns hat er seinem Volke kund gethan, indem er ihnen das Besitztum der Heiden verlieh.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Das Thun seiner Hände ist Treue und Recht; zuverlässig sind alle seine Befehle,
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 gestützt für immer, für ewig, ausgeführt in Treue und Redlichkeit.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Er hat seinem Volk Erlösung gesandt, auf ewig seinen Bund bestellt: heilig und furchtbar ist sein Name!
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Die Furcht Jahwes ist der Weisheit Anfang; gute Einsicht wird allen, die sie üben. Sein Lobpreis besteht für immer.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalm 111 >