< Sprueche 7 >

1 Mein Sohn, behalte meine Reden und verwahre meine Gebote bei dir.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Behalte meine Gebote, so wirst du leben, und meine Weisung wie deinen Augapfel.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Binde sie an deine Finger, schreibe sie auf die Tafel deines Herzens.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Sprich zur Weisheit: Meine Schwester bist du! und nenne Einsicht “Vertraute”,
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 daß du vor dem fremden Weibe bewahrt werdest, vor der Auswärtigen, die einschmeichelnd redet.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 Durch das Fenster nämlich meines Hauses, durch mein Gitter schaute ich aus.
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 Da sah ich unter den unerfahrenen, bemerkte unter den jungen Leuten einen unsinnigen Jüngling.
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 Der ging auf der Gasse, nahe einer Ecke, und schritt in der Richtung nach ihrem Hause einher.
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 In der Dämmerung am Abende des Tags, in schwarzer Nacht und Dunkelheit.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 Da auf einmal tritt ihm ein Weib entgegen im Huren-Anzug und mit heimtückischem Sinne -
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 leidenschaftlich ist sie und unbändig; ihre Füße können nicht im Hause bleiben.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Bald ist sie auf der Straße, bald auf den Plätzen und lauert neben jeder Ecke -
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 nun hat sie ihn gefaßt und geküßt; mit frecher Miene sprach sie zu ihm:
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 Heilsopfer lagen mir ob; heute habe ich meine Gelübde bezahlt.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 Darum bin ich herausgegangen, dir entgegen, um nach dir zu suchen, und habe dich nun gefunden.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 Mit Decken habe ich mein Bette bedeckt, mit buntgestreiften Teppichen von ägyptischem Garn.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 Ich habe mein Lager besprengt mit Balsam, Aloë und Zimmet.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Komm, wir wollen uns in Liebe berauschen bis zum Morgen, wollen schwelgen in Liebeslust.
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 Denn der Mann ist nicht daheim; er hat eine Reise in die Ferne angetreten.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 Den Geldbeutel hat er mit sich genommen; erst am Vollmondstage kehrt er wieder heim!
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 Durch ihr eifriges Zureden verführte sie ihn, riß ihn fort durch ihre glatten Lippen.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 Er folgt ihr plötzlich nach wie ein Stier, der zur Schlachtbank geführt wird, und wie ein Hirsch, der ins Netz rennt,
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 bis ihm der Pfeil die Leber spaltet; wie ein Vogel zur Schlinge eilt und weiß nicht, daß es sein Leben gilt.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 Nun denn, ihr Söhne, gehorcht mir und merkt auf die Reden meines Mundes.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Laß dein Herz nicht abbiegen zu ihren Wegen, verirre dich nicht auf ihre Steige.
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 Denn viel sind der Erschlagenen, die sie gefällt hat, und zahlreich sind, die sie alle gemordet hat.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Voller Wege zur Unterwelt ist ihr Haus, die hinabführen zu des Todes Kammern. (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Sprueche 7 >