< Job 9 >

1 Hiob antwortete und sprach:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Ja wohl, ich weiß, daß es so ist, - wie könnte der Mensch je Recht behalten gegen Gott!
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 Wenn er geruhte, mit ihm zu streiten, - nicht auf eins von Tausend könnt' er ihm erwidern!
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 Der weisen Sinnes und von gewaltiger Kraft ist - wer hat ihm je getrotzt und blieb unversehrt?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Er, der unvermerkt Berge versetzt, indem er sie umstürzt in seinem Grimm;
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 der die Erde aufbeben macht von ihrer Stätte, daß ihre Säulen ins Wanken geraten,
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 der der Sonne verbietet, aufzustrahlen, und die Sterne unter Siegel legt;
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 der den Himmel ausspannt allein und einher schreitet auf den Höhen des Meers,
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 der den Bären schuf, den Orion und die Pleiaden und die Kammern des Südens;
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 der große Dinge thut, die unerforschlich, und Wunder, die nicht aufzuzählen sind.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Fürwahr, er zieht an mir vorüber, aber ich sehe ihn nicht; er schwebt dahin, aber ich gewahre ihn nicht.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Rafft er hinweg, wer will ihm wehren? Wer darf zu ihm sprechen: “Was thust du da?”
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 Gott wehrt nicht seinem Zorn - krümmten sich doch Rahabs Helfer unter ihm! -
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 geschweige, daß ich ihm erwidern dürfte, ihm gegenüber meine Worte wählen könnte,
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 der ich, auch wenn ich Recht habe, keine Antwort bekomme, zu meinem Widerpart um Gnade flehen muß.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 Wenn ich ihn riefe und er gäbe mir Antwort, so würde ich's doch nicht glauben, daß er mich anhören werde.
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 Vielmehr, im Sturmwind würde er mich anschnauben und meine Wunden ohne Ursach' mehren,
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 würde mich nimmer aufatmen lassen, sondern mich sättigen mit bitterem Weh.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 Gilt's Kraft des Starken, so ist er da, aber gilt's den Rechtsweg - “wer darf mich vorfordern?”
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Wär' ich im Recht - mein Mund würde mich verdammen, wäre ich unschuldig - er würde mich zum Betrüger machen!
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Unschuldig bin ich - was kümmert mich mein Leben! ich verachte mein Dasein!
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 Eins ist es, drum spreche ich's aus: er bringt den Frommen wie den Frevler um!
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 Wenn die Geißel jählings tötet, so lacht er über die Verzweiflung Unschuldiger.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 Die Erde ist in der Frevler Hand gegeben, die Augen ihrer Richter hält er zu: wenn er nicht - wer denn sonst?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 und meine Tage eilten schneller dahin, als ein Läufer, entflohen, ohne Glück geschaut zu haben,
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 fuhren dahin wie Binsenkähne, wie ein Adler, der auf Beute stößt.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 Wenn ich denke: Ich will meinen Jammer vergessen, will meinen Unmut lassen und heiter blicken,
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 so schaudre ich vor allen meinen Schmerzen: ich weiß, daß du mich nicht lossprechen wirst.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Ich, ich soll schuldig sein, wozu mich da noch vergeblich abmühen?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 Wenn ich mich auch mit Schnee wüsche und meine Hände mit Lauge reinigte,
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 so würdest du mich in den Pfuhl eintauchen, daß meine Kleider vor mir Abscheu hätten.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 Denn er ist nicht ein Mensch wie ich, daß ich ihm Antwort geben, daß wir miteinander vor Gericht treten könnten.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 Kein Schiedsmann ist zwischen uns, der auf uns beide seine Hand legen könnte.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Er nehme seinen Stock von mir hinweg und lasse seinen Schrecken mich nicht ängstigen,
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 so will ich reden, ohne ihn zu fürchten, denn so steht es mit meinem Innern nicht!
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >