< Job 5 >

1 Rufe nur! Giebt's einen, der dir Antwort gäbe? und an wen unter den Heiligen wolltest du dich wenden?
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 Denn den Thoren mordet sein Unmut, und den Albernen tötet sein Eifern.
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 Ich habe einen Thoren festgewurzelt gesehen, verwünschte aber plötzlich seine Stätte.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 Seinen Kindern bleibt die Hilfe fern; sie müssen sich zertreten lassen im Thor, und keiner errettet sie.
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 Seine Ernte verzehrt der Hungrige - selbst aus den Dornen holt er sie heraus - und Durstige schnappen nach seinem Gut.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 Denn Unheil wächst nicht aus dem Staub hervor, noch sprießt das Elend aus dem Boden:
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 Nein, der Mensch ist zum Elend geboren, so wie der Flamme Kinder aufwärts fliegen.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 Ich aber würde mich an den Allmächtigen wenden und meine Sache Gott vorlegen,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 der große Dinge thut, die unerforschlich, und Wunder, die unzählbar sind:
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 Der der Erde Regen schenkt und Wasser auf die Fluren sendet,
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 der Niedrige hoch emporhebt, und Trauernde erfahren hohes Heil.
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 Er vereitelt die Pläne der Listigen, daß ihre Hände nichts Beständiges schaffen.
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 Er fängt die Klugen in ihrer eignen List, und der Verschlagenen Anschlag überstürzt sich.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 Am hellen Tage stoßen sie auf Finsternis und wie zur Nachtzeit tappen sie am Mittag.
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 So rettet er vom Schwert, aus ihrem Rachen, und aus der Gewalt des Starken den Armen.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 So geht dem Schwachen Hoffnung auf, und die Bosheit schließt ihr Maul.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 O, glücklich der Mann, den Gott zurechtweist! - so verschmähe nicht die Zucht des Allmächtigen!
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 Denn er verwundet, doch er verbindet auch; er zerschlägt, und seine Hände heilen.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 Aus sechs Nöten errettet er dich, und in sieben trifft dich kein Unheil.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 Bei Hungersnot errettet er dich vom Tode und im Kriege von den Streichen des Schwerts.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 Vor der Zunge Geißel bist du geborgen, hast nichts zu fürchten, wenn Verheerung naht.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 Der Verheerung und der Teuerung kannst du lachen, die wilden Tiere brauchst du nicht zu fürchten.
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 Denn mit des Feldes Steinen bist du im Bunde, und die wilden Tiere sind mit dir befreundet.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 Und so wirst du erfahren, daß wohlbehalten dein Zelt: du musterst deine Behausung und vermissest nichts.
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 Du wirst erfahren, daß deine Nachkommen zahlreich sind, und deine Sprossen wie das Gras der Flur.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 In Vollreife gehst du zum Grabe ein, gleichwie die Garbe hinaufgebracht wird zu ihrer Zeit.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Siehe, das ist's, was wir erforscht, so ist's! Vernimm es und beherzige es wohl!
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< Job 5 >