< Job 40 >

1 Und Jahwe antwortete Hiob und sprach:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Hadern mit dem Allmächtigen will der Tadler? Der Ankläger Gottes antwortete darauf!
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Dann antwortete Hiob Jahwe und sprach:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Fürwahr, zu gering bin ich; was soll ich dir erwidern? Ich lege meine Hand auf meinen Mund.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Einmal habe ich geredet und werde es nicht wiederholen - ein zweites Mal, und werde es nicht wieder thun!
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Dann antwortete Jahwe Hiob aus Wettersturm und sprach:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Auf, gürte deine Lenden wie ein Mann: Ich will dich fragen und du belehre mich!
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Willst du gar mein Recht zunichte machen, mich verdammen, damit du Recht behaltest?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Hast du denn einen Arm wie Gott und vermagst du mit gleichem Schall wie er zu donnern?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Schmücke dich doch mit Majestät und Hoheit! Umkleide dich mit Glanz und Herrlichkeit!
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Laß sich ergießen deines Zornes Fluten und wirf mit einem Blicke jeden Stolzen nieder!
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Mit einem Blicke demütige jeden Stolzen und strecke die Gottlosen zu Boden.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Birg sie im Staube allzumal, banne ihr Angesicht an verborgenem Ort,
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 so will auch ich dich loben, daß deine Rechte dir Sieg verschafft!
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Sieh nur das Nilpferd, das ich schuf wie dich; Gras frißt es wie ein Rind!
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Sieh nur seine Kraft in seinen Lenden und seine Stärke in den Muskeln seines Leibes.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Es streckt seinen Schwanz wie eine Ceder aus, die Sehnen seiner Schenkel sind dicht verschlungen.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Seine Knochen sind Röhren von Erz, seine Gebeine wie ein eiserner Stab.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Das ist der Erstling von Gottes Walten; der es schuf, reicht dar sein Schwert.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Denn Futter tragen ihm die Berge, wo alle Tiere des Feldes spielen.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Unter Lotusbüschen lagert es, im Versteck von Rohr und Schilf.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Lotusbüsche überdachen es, um ihm Schatten zu geben, des Baches Weiden umfangen es.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Wenn der Strom anschwillt, bangt es nicht, bleibt ruhig, wenn ein Jordan gegen seinen Rachen andringt.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Vermag es einer von vorn zu packen, mit Sprenkeln ihm die Nase zu durchbohren?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >