< Job 40 >

1 Und Jahwe antwortete Hiob und sprach:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Hadern mit dem Allmächtigen will der Tadler? Der Ankläger Gottes antwortete darauf!
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Dann antwortete Hiob Jahwe und sprach:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Fürwahr, zu gering bin ich; was soll ich dir erwidern? Ich lege meine Hand auf meinen Mund.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Einmal habe ich geredet und werde es nicht wiederholen - ein zweites Mal, und werde es nicht wieder thun!
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Dann antwortete Jahwe Hiob aus Wettersturm und sprach:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Auf, gürte deine Lenden wie ein Mann: Ich will dich fragen und du belehre mich!
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Willst du gar mein Recht zunichte machen, mich verdammen, damit du Recht behaltest?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hast du denn einen Arm wie Gott und vermagst du mit gleichem Schall wie er zu donnern?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Schmücke dich doch mit Majestät und Hoheit! Umkleide dich mit Glanz und Herrlichkeit!
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Laß sich ergießen deines Zornes Fluten und wirf mit einem Blicke jeden Stolzen nieder!
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Mit einem Blicke demütige jeden Stolzen und strecke die Gottlosen zu Boden.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Birg sie im Staube allzumal, banne ihr Angesicht an verborgenem Ort,
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 so will auch ich dich loben, daß deine Rechte dir Sieg verschafft!
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Sieh nur das Nilpferd, das ich schuf wie dich; Gras frißt es wie ein Rind!
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Sieh nur seine Kraft in seinen Lenden und seine Stärke in den Muskeln seines Leibes.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Es streckt seinen Schwanz wie eine Ceder aus, die Sehnen seiner Schenkel sind dicht verschlungen.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Seine Knochen sind Röhren von Erz, seine Gebeine wie ein eiserner Stab.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Das ist der Erstling von Gottes Walten; der es schuf, reicht dar sein Schwert.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Denn Futter tragen ihm die Berge, wo alle Tiere des Feldes spielen.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Unter Lotusbüschen lagert es, im Versteck von Rohr und Schilf.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Lotusbüsche überdachen es, um ihm Schatten zu geben, des Baches Weiden umfangen es.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Wenn der Strom anschwillt, bangt es nicht, bleibt ruhig, wenn ein Jordan gegen seinen Rachen andringt.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Vermag es einer von vorn zu packen, mit Sprenkeln ihm die Nase zu durchbohren?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >