< Job 28 >

1 Wohl giebt es einen Fundort für das Silber, eine Stätte für das Gold, das man läutert.
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 Eisen wird aus dem Erdreiche geholt, und Gestein schmilzt man zu Erz.
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Ein Ende hat man der Finsternis gemacht und bis zur äußersten Grenze durchforscht man das im tiefsten Dunkel verborgene Gestein.
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 Man bricht einen Schacht fern von den droben Wohnenden; vergessen von dem droben schreitenden Fuß, fern von den Menschen hangen, schweben sie.
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 Aus der Erde geht Brotkorn hervor, und ihr Tiefen werden wie mit Feuer umgewühlt.
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 Des Saphirs Fundstätte ist ihr Gestein, Goldstäubchen werden ihm zu teil.
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 Den Weg kennt nicht der Adler, noch erspäht ihn des Geiers Auge.
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 Nicht betreten ihn die stolzen Raubtiere, noch schreitet auf ihm der Leu.
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 An den Kiesel legt man die Hand, wühlt von Grund aus die Berge um.
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 Durch die Felsen schlägt man Gänge, und allerlei Kostbares erschaut das Auge.
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 Die Wasseradern verbindet man, daß sie nicht thränen, und bringt Verborgenes ans Licht.
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 Die Weisheit aber, wo findet man sie, und wo ist der Fundort der Erkenntnis?
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Kein Mensch kennt den Weg zu ihr, und sie ist nicht zu finden im Lande der Lebendigen.
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Die Meerestiefe spricht: “In mir ist sie nicht!” und das Meer spricht: “Sie ist nicht bei mir!”
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 Mit gediegenem Golde wird sie nicht erkauft, noch wird Silber dargewogen als ihr Preis.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Sie läßt sich nicht aufwiegen mit Ophirgold, mit kostbarem Schoham und Sapphir.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Gold und Glas kommen ihr nicht gleich, noch tauscht man sie ein für güldenes Geschirr.
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 Korallen und Krystall kommen nicht in Betracht, und der Besitz der Weisheit geht über Perlen.
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 Äthiopiens Topas kommt ihr nicht gleich, mit reinstem Golde wird sie nicht aufgewogen.
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 Die Weisheit also - woher kommt sie, und wo ist der Fundort der Erkenntnis?
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 Verhüllt ist sie vor den Augen aller Lebenden, auch den Vögeln unter dem Himmel ist sie verborgen.
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Abgrund und Tod sprechen: “Wir haben mit unseren Ohren ein Gerücht von ihr gehört.”
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 Gott kennt den Weg zu ihr und er weiß um ihren Fundort.
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 Denn er schaut bis zu der Erde Enden; was irgend unter dem Himmel ist, sieht er.
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 Als er des Windes Wucht abwog und dem Wasser sein Maß bestimmte,
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 als er dem Regen sein Gesetz gab, und seinen Pfad dem Wasserstrahle,
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 da sah er sie und machte sie kund, stellte sie hin und durchforschte sie.
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 Und zum Menschen sprach er: Siehe, Furcht des Herrn, das ist Weisheit, und das Böse meiden, ist Verstand!
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”

< Job 28 >