< Job 16 >

1 Hiob antwortete und sprach:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Dergleichen habe ich vieles gehört, leidige Tröster seid ihr insgesamt.
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Sind die windigen Reden nun zu Ende? oder was reizt dich zum Erwidern?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 Auch ich könnte sprechen wie ihr, wäre euch nur zu Mute, wie mir zu Mute ist, könnte Reden wider euch zusammendrechseln und den Kopf über euch schütteln,
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 euch stärken mit meinem Mund, und meiner Lippen Beileid sollte lindern!
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Mag ich reden - mein Schmerz wird nicht gelindert, und unterlasse ich's - was wird dann von mir weichen?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 Hat er doch nunmehr meine Kraft erschöpft - verödet hast du meinen ganzen Kreis,
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 hast mich gepackt, das muß als Zeugnis gelten! Mein eignes Siechtum tritt wider mich auf, ins Angesicht hinein verklagt es mich.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 Sein Grimm zerfleischt und befehdet mich, er fletscht gegen mich seine Zähne; als mein Widersacher wetzt er seine Augen wider mich.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 Man reißt gegen mich das Maul auf, schlägt mich schmählich auf die Wangen; insgesamt rotten sie sich gegen mich zusammen.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 Gott giebt mich Frevlern preis und in der Gottlosen Hände stürzt er mich.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 Ich lebte ruhig, da zerschmetterte er mich, packte mich beim Genick und schüttelte mich und stellte mich als Zielscheibe für sich auf.
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 Es umschwirren mich seine Pfeile; erbarmungslos spaltet er meine Nieren, gießt auf die Erde meine Galle.
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 Bresche auf Bresche legt er in mich, stürmt gegen mich an wie ein Kriegsheld.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 Härenes Gewand habe ich um meine Haut genäht, habe in den Staub mein Horn gebohrt.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 Mein Antlitz ist hochgerötet vom Weinen, und tiefes Dunkel ruht auf meinen Wimpern,
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 obwohl kein Frevel an meinen Händen, und mein Gebet lauter ist.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O Erde, bedecke nicht mein Blut! Mein Wehruf finde keine Ruhestatt!
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Schon jetzt ist im Himmel mein Zeuge, und mein Bürge in der Höhe.
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 Meine Freunde spotten mein - zu Gott blickt thränend mein Auge empor,
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 daß er dem Manne Recht schaffe gegen Gott und zwischen dem Menschen und seinem Freund entscheide.
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 Denn nur noch wenige Jahre werden kommen, und den Pfad ohne Rückkehr muß ich wandeln.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Job 16 >