< Job 13 >

1 Sieh', alles hat mein Auge gesehen, mein Ohr gehört und sich's gemerkt!
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 Was ihr wißt, weiß ich auch; ich stehe hinter euch nicht zurück.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 Aber ich will zum Allmächtigen reden und mit Gott zu rechten habe ich Lust.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 Denn wahrlich, ihr seid Lügenschmiede und Flicker von Nichtigem insgesamt.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 O daß ihr doch ganz stille schwiegt, so könnte das als eure Weisheit gelten!
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 So hört denn die Rüge meines Mundes und merkt auf die Vorwürfe meiner Lippen.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Wollt ihr Gott zu Liebe Unrecht reden und ihm zu Liebe Trug reden?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Wollt ihr für ihn Partei ergreifen oder für Gott streiten?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Wird es gut ablaufen, wenn er euch erforscht, oder wollt ihr ihn narren, wie man Menschen narrt?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 Nein, strafen, strafen wird er euch, wenn ihr insgeheim Partei ergreift.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Seine Hoheit wird euch betäuben, und sein Schrecken auf euch fallen.
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Eure Merksprüche sind Aschensprüche, Lehmschanzen sind eure Schanzen.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 Laßt mich in Ruhe, so will ich reden, mag über mich ergehen, was da will.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Ich will mein Fleisch in meine Zähne nehmen und mein Leben aufs Spiel setzen.
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Er wird mich töten - ich harre seiner; nur will ich meinen Wandel ihm ins Angesicht darlegen.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 Schon das gereicht mir zum Sieg, daß vor sein Angesicht kein Heuchler tritt.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 So hört denn aufmerksam meine Rede, und meine Darlegung dringe zu euren Ohren.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Wohlan, ich habe den Handel eingeleitet; ich weiß, daß ich Recht behalten werde.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Wer ist's, der mit mir streiten dürfte? - denn dann wollt' ich schweigen und verscheiden!
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 Nur zweierlei thue mir nicht an, dann will ich mich vor deinem Antlitz nicht verbergen:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 Zieh deine Hand von mir zurück und laß deinen Schrecken mich nicht ängstigen;
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 dann rufe, so will ich Rede stehn, oder ich will reden, und du entgegne mir!
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 Wieviel Vergehungen und Sünden habe ich denn? Meinen Frevel und meine Sünde laß mich wissen!
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Warum verhüllst du dein Antlitz und erachtest mich für deinen Feind?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Willst du ein verwehtes Blatt aufschrecken und den dürren Halm verfolgen,
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 daß du mir Bitteres als Urteil schreibst und mich die Sünden meiner Jugend erben lässest?
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 daß du meine Füße in den Block legst und alle meine Wege bewachst und dir einen Kreis um meine Sohlen ziehst?
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 Und eben dieser Mann zerfällt wie von Wurmfraß, wie ein Kleid, das die Motte zerfressen hat!
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.

< Job 13 >