< 1 Mose 5 >

1 Dies ist das Buch über die Nachkommen Adams. Als Gott den Adam erschuf, da erschuf er ihn Gott ähnlich;
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 als Mann und Weib erschuf er sie und er segnete sie und gab ihnen den Namen “Mensch” damals, als sie geschaffen wurden.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Als nun Adam 130 Jahre alt war, erzeugte er einen Sohn, der ihm glich als sein Abbild, und gab ihm den Namen Seth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 Nach der Erzeugung des Seth aber lebte Adam noch 800 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 Und die ganze Lebensdauer Adams, die er durchlebte, betrug 930 Jahre; sodann starb er.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Als nun Seth 105 Jahre alt war, erzeugte er den Enos.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Nach der Erzeugung des Enos aber lebte Seth noch 807 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 Und die ganze Lebensdauer Seths betrug 912 Jahre; sodann starb er.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Als nun Enos 90 Jahre alt war, erzeugte er den Kenan.
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Nach der Erzeugung Kenans aber lebte Enos noch 815 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 Und die ganze Lebensdauer des Enos betrug 905 Jahre; sodann starb er.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Als nun Kenan 70 Jahre alt war, erzeugte er den Mahalalel.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Nach der Erzeugung Mahalalels aber lebte Kenan noch 840 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Und die ganze Lebensdauer Kenans betrug 910 Jahre; sodann starb er.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Als nun Mahalalel 65 Jahre alt war, erzeugte er den Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 Nach der Erzeugung Jareds aber lebte Mahalalel noch 830 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 Und die ganze Lebensdauer Mahalalels betrug 895 Jahre; sodann starb er.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 Als nun Jared 162 Jahre alt war, erzeugte er den Henoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 Nach der Erzeugung Henochs aber lebte Jared noch 800 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Und die ganze Lebensdauer Jareds betrug 962 Jahre; sodann starb er.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Als nun Henoch 65 Jahre alt war, erzeugte er den Methusalah.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 Nach der Erzeugung Methusalahs aber wandelte Henoch in Gemeinschaft mit Gott 300 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 Und die ganze Lebensdauer Henochs betrug 365 Jahre.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 Und weil Henoch in Gemeinschaft mit Gott gewandelt hatte, so verschwand er einst, denn Gott hatte ihn hinweggenommen.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Als nun Methusalah 187 Jahre alt war, erzeugte er den Lamech.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 Nach der Erzeugung des Lamech aber lebte Methusalah noch 782 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 Und die ganze Lebensdauer Methusalahs betrug 969 Jahre; sodann starb er.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Als nun Lamech 182 Jahre alt war, erzeugte er einen Sohn;
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 den hieß er Noah, indem er sprach: Dieser wird uns aufatmen lassen von unserer Arbeit und der Mühsal unserer Hände, die uns verursacht wird von dem Boden, den Jahwe verflucht hat!
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 Nach der Erzeugung Noahs aber lebte Lamech noch 595 Jahre und erzeugte Söhne und Töchter.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 Und die ganze Lebensdauer Lamechs betrug 777 Jahre; sodann starb er.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 Als nun Noah 500 Jahre alt war, erzeugte er den Sem, den Ham und den Japhet.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< 1 Mose 5 >