< 1 Mose 10 >

1 Und dies ist die Geschichte der Söhne Noahs, Sem, Ham und Japhet; und es wurden ihnen Söhne geboren nach der Flut.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Die Söhne Japhets waren: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Mesech und Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Und die Söhne Gomers: Askenas, Riphath und Togarma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Und die Söhne Javans: Elisa, Tarsis, die Kittiter und die Rodaniter.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Von diesen zweigten sich ab die Bewohner der Inseln der Heiden. Dies sind die Söhne Japhets nach ihren Ländern, ihren verschiedenen Sprachen, ihren Stämmen, ihren Völkerschaften.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Und die Söhne Hams waren Kusch, Mizraim, Put und Kanaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 Und die Söhne Kuschs: Seba, Havila, Sabta, Raema und Sabtecha; und die Söhne Raemas waren Saba und Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Und Kusch erzeugte den Nimrod; dieser fing an, ein Gewaltiger zu werden auf der Erde.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 Dieser war ein gewaltiger Jäger vor Jahwe; daher pflegt man zu sagen: ein gewaltiger Jäger vor Jahwe, wie Nimrod!
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Es erstreckte sich aber seine Herrschaft anfänglich auf Babel und Erech und Akkad und Kalne im Lande Sinear.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Von diesem Lande zog er aus nach Assur und erbaute Nineve und Rehoboth-Ir und Kalah
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 und Resen zwischen Nineve und Kalah - das ist die große Stadt.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Und Mizraim erzeugte die Luditer, die Anamiter, die Lehabiter, die Naphtuhiter,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 die Patrusiter, die Kasluhiter (von denen die Philister ausgegangen sind) und die Kaphtoriter.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kanaan aber erzeugte Sidon, seinen Erstgebornen, und Heth
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 und die Jebusiter, Amoriter, Girgasiter,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Heviter, Arkiter, Siniter,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Arvaditer, Zemariter und Hamathiter; und darnach breiteten sich die Stämme der Kanaaniter aus.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 Und das Gebiet der Kanaaniter erstreckte sich von Zidon bis hin nach Gerar bis Gaza, bis hin nach Sodom, Gomorra, Adma und Zeboim bis Lasa.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Dies sind die Söhne Hams nach ihren Stämmen und Sprachen, ihren Ländern und Völkerschaften.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Aber auch Sem, dem Stammvater aller Söhne Ebers, dem älteren Bruder Japhets, wurden Söhne geboren.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Die Söhne Sems sind Elam, Assur, Arpachsad, Lud und Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Und die Söhne Arams sind Uz, Hul, Gether und Mas.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Arpachsad aber erzeugte Selah und Selah erzeugte Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Und dem Eber wurden zwei Söhne geboren; der eine hieß Peleg, weil sich zu seiner Zeit die Bevölkerung der Erde zerteilte, und sein Bruder hieß Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Und Joktan erzeugte Almodad, Saleph, Hazarmaveth, Jarah,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Usal, Dikla,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Saba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Havila und Jobab: diese alle sind Söhne Joktans.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Und ihre Wohnsitze erstreckten sich von Mesa bis gen Sephar, bis zum Ostgebirge.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Das sind die Söhne Sems nach ihren Stämmen und Sprachen, ihren Ländern und Völkerschaften.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Das sind die Stämme der Söhne Noahs nach ihren Sippschaften, ihren Völkern; und von ihnen zweigten sich ab die Völker auf Erden nach der Flut.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< 1 Mose 10 >