< Psalm 72 >

1 Von Salomo. - Gott, gib dem König Deine Ordnungen, dem Königssohn Dein Recht,
Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
2 daß er Dein Volk gemäß dem Rechte richte und Deine Armen nach Gerechtigkeit!
Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
3 Die Berge laß dem Volke Frieden bringen, Gerechtigkeit die Hügel!
Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
4 Er schaffe Recht den Elenden im Volk und helfe armer Leute Kindern! Doch den Bedrücker möge er zermalmen!
Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
5 Er lebe auch, solange Mond und Sonne währen!
Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
6 Er komme wie der Regen auf die abgemähte Flur, wie Regengüsse auf das Land!
Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
7 In seinen Tagen blühe auf der Fromme, und Friedensfülle sei, bis nimmer ist der Mond!
Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
8 Von Meer zu Meere herrsche er, vom Strom bis an der Erde Enden!
Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
9 Seemächte sollen sich vor ihm erniedrigen und seine Feinde Staub auflecken!
Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
10 Die Könige von Tarsis und die der Inseln sollen Gaben bringen, Tribut die Könige von Saba und von Seba
Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
11 und alle Könige ihm huldigen! Ihm sollen alle Heidenvölker dienstbar sein!
Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
12 Den Armen rettet er, wenn er um Hilfe ruft, den Leidenden, der keinen Beistand hat.
Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
13 Er schont den Armen und Geringen und rettet der Bedrückten Leben.
Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
14 Von Schaden und Gewalt erlöst er ihre Seele; denn teuer achtet er ihr Blut.
Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 Man rufe alsdann "Lebe hoch!" Er gibt dafür von Sabas Golde, damit für ihn bete, ihn beständig segne!
Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
16 Er sei ein Fruchtgefilde auf der Erde! Auf Bergesgipfeln, gleich dem Libanon, da woge auch noch seine Frucht! Sie sprosse aus der Stadt wie Pflanzen aus der Erde!
Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
17 Sein Name währe ewiglich! Solange eine Sonne ist, so währe auch sein Name! Daß alle Heiden ihn beim Segnen nennen und glücklich preisen! -
Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
18 Gepriesen sei der Herr und Gott, der Schutzgott Israels, der einzig Wunder tut!
Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
19 Gepriesen sei der Name seines Herrschertums in Ewigkeit! Die ganze Erde sei erfüllt von seiner Herrlichkeit! Amen! Amen! -
Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
20 Zu Ende sind die Gebete Davids, des Isaisohnes.
Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

< Psalm 72 >