< Psalm 50 >

1 Ein Lied, von Asaph. - Gott, Gott der Herr, soll reden; rufe er die Erde vom Aufgang bis zum Niedergang!
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 Von Sion her, der Schönheit Krone, erstrahle Gott!
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 So komme wieder unser Gott und schweige nicht! Verzehrend Feuer schreite vor ihm her; gewaltig stürme es um ihn!
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 Dem Himmel droben rufe er und dann der Erde mit den Worten:
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 "Versammelt mir jetzt meine Frommen, die einen Bund mit mir geschlossen!", daß sie sein Volk der Opfer wegen richten.
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Der Himmel lege Zeugnis dafür ab: "Er ist im Recht; er ist ein Gott des Rechtes." (Sela)
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 Mein Volk, gib acht und laß mich reden, Israel! Dich ermahn ich ernstlich: "Gott, dein Gott, bin ich.
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Ich tadle dich nicht deiner Opfer wegen, und deine Brandopfer steht immer mir vor Augen.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Doch brauche ich kein Rind aus deinem Hause, aus deinen Hürden keine Böcke.
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 Denn mein ist alles Wild im Walde, auf Tausenden von Bergen das Getier.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Ich kenne alle Vögel im Gebirge; mir steht zu Diensten das, was sich im Felde regt.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Und sollte je ich hungern, dir sagt' ich es nicht; mein ist die Welt und was sie füllt.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Will ich denn Fleisch von Stieren essen? Und trinke ich der Böcke Blut?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Bring Dank dem Herrn zum Opfer dar und löse so dem Höchsten dein Gelübde!
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 Und ruf am Tag der Not mich an. Dann werde ich dich retten. Aber danken sollst du mir."
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Zum Frevler aber spreche Gott: "Was schwatzest du von meinen Satzungen und führst im Munde meinen Bund!
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 Du hassest doch die Zucht, und meine Worte schlägst du in den Wind.
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Kaum siehst du einen Dieb, so läufst du schon mit ihm. Mit Ehebrechern gehst du um
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 und lässest deinen Mund in Bosheit sich ergehen, und deine Zunge paarest du mit Trug.
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 Da setzst du dich und redest gegen deinen Bruder, verleumdest deiner Mutter Sohn.
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Das tust du, und ich sollte schweigen? Du dächtest dann, ich sei wie du. Zur Rede stelle ich dich jetzt und zeige deutlich dir den Unterschied-
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 Dies merkt, ihr Gottvergessenen! Sonst raffe ich euch rettungslos dahin.
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 Wer Dank darbringt, der gibt mir Ehre. Wer gutes Beispiel gibt, den laß' ich göttlich Heil erblicken."
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

< Psalm 50 >