< Psalm 33 >

1 Ihr Frommen, jauchzt dem Herrn! Den Redlichen ziemt Lobgesang.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 Mit Zitherklängen dankt dem Herrn! Ihm spielt auf Harfen mit zehn Saiten!
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 Ihm singt ein nie gehörtes Lied! Und schlaget kräftig in die Saiten, daß es schallt!
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Wahrhaftig ist das Wort des Herrn, und Treue ist sein ganzes Tun.
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 Er liebt Gerechtigkeit und Recht; des Herrn Güte ist die Erde voll.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Die Himmel sind geworden durch das Wort des Herrn, durch seines Mundes Hauch ihr ganzes Heer.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Er sammelt wie in einen Schlauch ein Meer von Wasser und legt in Speicher Ozeane.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 So fürchte alle Welt sich vor dem Herrn! Vor ihm erschauere jeder Erdbewohner!
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 Denn so er spricht, geschieht's, gebietet er's, so bleibt es aus.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 Zunichte macht der Herr der Heiden Plan; der Völker Absichten vereitelt er.
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 Der Plan des Herrn ist unveränderlich, und seines Herzens Pläne gelten für und für.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Heil sei dem Heidenvolke, dessen Gott der Herr, der Nation, die er zur ewig Seinen sich erkoren!
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 Vom Himmel schaut der Herr herab und blickt auf alle Menschenkinder!
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 Von seiner Wohnstatt schaut er nieder auf alle Erdbewohner.
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 Ihm, der geschaffen ihre Herzen allzumal, dem ist bekannt ihr ganzes Tun.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 Kein König siegt durch Heeresmacht; den Riesen rettet nicht die Fülle seiner Kraft.
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 Betrogen, wer vom Roß den Sieg erwartet; nicht Rettung bringt es ihm trotz großer Stärke.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Auf denen, so ihn fürchten, ruht des Herrn Auge, auf denen, die von seiner Güte hoffen,
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 daß er vor Pest ihr Leben rette und sie in Hungersnot erhalte.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 Dem Herrn gilt unserer Seele Harren; uns ist er Schutz und Schild.
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 So froh wird unser Herz durch ihn; denn wir vertrauen seinem heiligen Namen.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Herr! Deine Gnade walte über uns, so wie wir sie von Dir erhoffen!
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.

< Psalm 33 >