< Psalm 135 >

1 Alleluja! Lobpreist des Herren Namen! Lobpreist ihn ihr, des Herren Diener,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 die ihr im Haus des Herren weilet, in unseres Gotteshauses Höfen!
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Singt Alleluja! Denn der Herr ist gut. Singt seinem Namen! Er ist liebreich,
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 hat doch der Herr sich Jakob auserkoren, zu seinem Eigentum sich Israel. -
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Ich weiß, der Herr ist so gewaltig, daß unser Herr die Götter alle überragt.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Der Herr tut, was er will, im Himmel und auf Erden, im Meer und in den Tiefen all.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Der Du heraufführst Wolken von der Erde Ende und Blitze für den Regen bildest, der Du den Wind aus seinen Kammern lässest,
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 der Du die Erstgeburt Ägyptens schlugest, vom Menschen bis zum Vieh,
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 und in Ägypten wunderbare Zeichen an Pharao und allen seinen Knechten tatest
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 und große Völker niederschlugst und starke Könige vertilgtest,
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 den Amoriterkönig Sichon, den Basankönig Og und alle Reiche Kanaans
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 und deren Land zum ewigen Besitze machtest, zum ewigen Besitze Deines Volkes Israel.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Dein Name ist auf ewig "Herr", für alle Zeiten wirst Du "Herr" genannt. -
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Der Herr schafft seinem Volke Recht, erbarmt sich seiner Diener.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Der Heiden Götzen sind von Gold und Silber, der Menschenhände Werk.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Sie haben einen Mund und reden nicht und Augen, doch sie sehen nicht.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Nicht hören sie mit ihren Ohren; kein Odem ist in ihrem Mund.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Wie sie, so sollen werden, die sie machen, und so, wer sich auf sie verläßt! -
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Lobpreis den Herrn, Haus Israel! Du Aaronshaus, Lobpreis den Herrn!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Du Levis Haus, Lobpreis den Herrn! Die ihr den Herrn fürchtet, preist den Herrn!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Gepriesen sei der Herr von Sion aus, der thronet zu Jerusalem! Alleluja!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalm 135 >