< Psalm 111 >

1 Alleluja! Aus ganzem Herzen danke ich dem Herrn im Kreis der Frommen und in der Gemeinde.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Des Herren Werke sind gewaltig, wie ausgesucht für alle ihre Zwecke.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Sein Wirken ist nur Pracht und Glanz, und ewig währet seine Liebe.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 Er sorgt für seiner Wunder Fortbestand; erbarmungsvoll und gnädig ist der Herr.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Er spendet Nahrung denen, die ihn fürchten, auf immer seines Bundes eingedenk.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 Er zeigte seinem Volke seiner Taten höchstes Maß, wie er das Eigentum der Heiden ihnen zum Besitze gab.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Von Recht und Treue zeugt ja seiner Hände Werk; was er verfügt, ist alles wohlgemeint.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 Für alle Zeiten sind sie festgesetzt und ausgeführt mit Treue und Gerechtigkeit.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Er sandte seinem Volk Erlösung und schloß auf ewig seinen Bund. "Furchtbarer", "Heiliger" ist sein Name.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Der Weisheit Anfang ist die Furcht des Herrn. Wer also tut, der führt sich gut. Sein Ruhm besteht für ewige Zeiten.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalm 111 >