< Psalm 1 >

1 Heil sei dem Mann, der nach der Frevler Rat nicht wandelt, nicht auf dem Weg der Sünder bleibt, nicht in der Spötter Runde weilt,
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 den nur des Herren Lehre freut, der seine Lehre Tag und Nacht betrachtet!
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Er grünet wie der Baum, verpflanzt an Wasserbäche, der Früchte trägt zur rechten Zeit, und dessen Laub nicht welkt. Und was er tut, gerät ihm gut.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 Nicht so die Frevler! Sie sind wie Spreu, die jeder Wind verweht.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Drum halten Frevler nicht in dem Gerichte stand; die Sünder sind nicht bei der Frommen Sammlung.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 Der Frommen Weg: des Herren Sorge; der Frevler Weg: der Untergang.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Psalm 1 >